News
Manchester United Guu Moja Fainali Europa

Miamba wa Uingereza kilabu ya manchester united imeweka guu moja fainali ya UEFA Europa Ligi baada ya ushindi wao mnono wa magoli 3-0 dhidi ya Athletic Bilbao ugani san mames uhispania.
Kiungo wa taifa la Brazil Casemiro aliwaweka uongozi Mashetani wekundu kunako dakika 30 kipindi cha kwanza kabla ya nahodha Bruno Fernandes kuongeza goli la pili dakika ya 37 huku akifunga lingine na lake la pili dakika ya 45 kupitia tuta au penalty.
Kilabu ya Bilbao walimaliza wachezaji 10 baada ya kadi nyekundu kwa beki wake Dani vivian dakika ya 35. kwenye mechi nyingine Tottenham Hotspurs walicharaza Bodo/Glimt ya Norway magoli 3-1.
Kwenye taji la Uefa Conference ligi kilabu ya Chelsea ilichapa Djugarden ya uswedi magoli 4-1 nayo Real Betis ya Uhispania ikichakaza Fiorentina ya Italia magoli 2-1 .
Mechi za mkondo wa pili utapigwa Alhamisi ijayo ugani Old Trafford ambapo Bilbao itahitaji kuwafunga United magoli 4-0 ili kufuzu kwenye fainali Mei 21.
News
Aisha Jumwa akosolewa kutokana na matamshi yake

Jopo la ushauri la viongozi na maimamu wa Takaungu wadi ya Mnarani kaunti ya Kilifi limeeleza kusikitishwa na kauli zilizotolewa na Aisha Jumwa kuhusiana na tukio la mauaji na maziko ya kijana mmoja eneo hilo lililomtaja kama Zakariyah Kirao Charo.
Likizungumza na vyombo vya habari, jopo hilo likiongozwa na sheikh Mahadh Ali wa msikiti Maryam limemkosoa Jumwa kwa kile lilichosema ameuhujumu uislamu kutokana na kauli alizotoa kwenye mtandao wake wa kijamii wa tiktok kuhusiana na mazishi ya kijana huyo.
Sheikh Mahadh amesema Jumwa alidai kuwa familia ya marehemu haikuhusishwa ilhali walichukua wajibu wa kuihusisha familia kabla ya hatua zozote kuchukuliwa ila wanafamilia wenyewe hawakuonyesha ushirikiano akieleza kuwa jopo hilo pia liligadhabishwa na kauli za Jumwa kuhusiana na namna mchakato mzima wa mazishi ulivyofanywa.
Akiunga mkono kauli hiyo Ustadh Mohamed Khamis amesema kwenye mkao huo kuwa amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa Jumwa tangia mtafuruku huo ulipoanza akisisitiza haja ya swala hilo kutotumika kwa namna ya kuchochea wanajamii waislamu na wasio kuwa waislamu katika eneo hilo la Takaungu.

Aisha Jumwa /Picha kwa hisani
Ustadh Mohamed pia amekinzana na kauli kuwa marehemu alisilimishwa akiwa na matatizo ya kiakili akisema ni sharti swala hilo lisiingiziwe siasa.
News
Viongozi wa Kilifi Wapinga Uekezaji wa Mradi wa Kawi ya Nuklia

Wizara ya Kawi nchini imefanya kikao cha mazungumzo na uongozi wa kaunti ya Kilifi, pamoja na wabunge na Wasimamizi wa Shirika la NUPEA kuhusu uekezaji wa mradi wa uzalishaji kawi ya Nuklia katika kijiji cha Uyombo wadi ya Matsangoni katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini katika kaunti ya Kilifi.
Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho mjini Kilifi, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi amesema japo viongozi wa kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi hawajaridhishwa na uekezaji wa mradi huo, mazungumzo kuhusu mradi huo bado yataendelea ili kuibuka na mwafaka kwani utasaidia pakubwa katika uzalishaji kawi.
Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema msimamo wa serikali ya kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi bado uko pale pale wa kuendelea kupinga uekezaji wa mradi huo wa mabilioni ya pesa, akisema utafiti uliofanywa umebaini kwamba mradi huo unaathari kubwa kwa wananchi.
Hata hivyo Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya amesema kama viongozi kutoka kaunti ya Kilifi hawako tayari kupokea mradi huo wa uzalishaji kawi ya Nuklia, akisema changamoto nyingi bado hazitatuliwa katika mradi huo ambazo ni athari kwa wananchi.
Kikao hicho hata hivyo kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Katibu katika Wizara ya masuala ya vijana na michezo nchini Fikirini Jacobs miongoni mwa viongozi wengine.