News
Wakaazi wa Nyari Wanapinga Uekezaji wa Madini

Wakaazi katika kijii cha Nyari eneo la Sokoke gatuzi dogo la Ganze kaunti ya Kilifi, wanakosoa mpango wa mwekezaji mmoja anayetaka kuchimba madini sehemu hiyo, wakidai kwamba hajahusisha umma.
Wakiongozwa na Thoya Sirya, wakaazi hao wameandamana wakisema wanatilia shaka mienendo ya mwekezaji huyo wa kampuni ya Jalin East Africa Mining ambayo huenda ikawakandamiza.
Wakaazi hao wamemkosoa mwekezaji huyo wakisema amekuwa akishinikiza wakaazi wa sehemu hiyo kutia saini makubaliano bila ya kuwapa mwelekeo wa fidia ya sehemu za ardhi zao.
Kulingana na wakaazi hao, mwekezaji huyo anapanga kuchimba madini aina ya Titanium ambayo jamii inafaa kufaidi kutokana na uekezaji huo.
News
Jopo la ushauri na Maimamu eneo la Takaungu lasisitiza Samuel Charo alisilimu kwa hiari yake

Jopo la ushauri na maimamu katika eneo la Takaungu wadi ya mnarani kaunti ya Kilifi limepinga madai yalioibuliwa na wanafamilia wa kijana aliyeuawa baada ya kumuua na kula matumbo ya mzee mmoja aliyekuwa ustadh aliyetambulika kama Ainen.
Kwa mujibu wa ustadh Abubakar Ratili wa masjid Answar kule Takaungu, marehemu Samuel Kirao Charo alisilimishwa na kupewa jina Zakariyah akisisitiza kuwa marehemu alisilimu kwa hiyari yake mbele ya waislam wengine kwenye msikiti huo
Aidha Sheikh Mahadh Ali ambaye pia ni imam wa msikiti Maryam eneo hilo la Takaungu pamoja na Ustadh Mohamed Khamis wameeleza kuwa dini ya kiislam inaruhusu mwili kuzikwa usiku akikashifu swala la kuhusisha hatua hiyo na ushirikina kama ilivyodaiwa na baadhi ya watu.
Jopo hilo pia limeeleza kuwa wanafamilia walihusishwa ila walidinda kushirikiana nao jambo lililopelekea jamii hiyo ya kiislamu kuendeleza maziko ya marehemu kwa mujibu wa Imani ya dini ya kiislam.
News
Wanaharakati na vijana wa Gen -z wazua purukushani kwenye majengo ya bunge la Mombasa
Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu na vijana wa Gen – Z katika kaunti ya Mombasa wemezuiwa kuingia katika bunge la kaunti ya Mombasa kuwasilisha malalamishi yao kuhusiana na bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2025/26.
Vijana hao pamoja na wanaharakati hao waliojawa na hasira wanasema wenyeji wa Mombasa hawajahusishwa kiukamilifu Katika mchakato huo tofauti na inavyofanyika kwenye kaunti zingine nchini.
Wanadai hali ya kutokuwa na uwazi katika utekelezaji wa miswada ya fedha kwenye kaunti hiyo kunachangia kwa shughuli mbalimbali kaunti ya Mombasa kukosa kutekelezwa ipasavyo
Hatahivyo baadae Karani wa bunge la kaunti ya Mombasa salim Juma alipokea malalamishi yao na kuahidi kutoa mwelekeo ufaao Jumanne wiki ijao huku vijana hao wakitishia kurudi tena iwapo malalamishi yao hayatatiliwa maanani.

Bunge la kaunti ya Mombasa/Picha kwa hisani