News
Ni Lazima Tushinde Paris Asema Arteta

Mkufunzi wa kilabu ya Arsenal Mikel Arteta angali na imani kwamba vijana wake watanyuka Psg ugenini na kufuzu kwenye fainali ya kilabu bingwa ulaya wiki ijayo mjini Paris.
Akizungumza baada ya The Gunners kukubali kichapo cha goli 1-0 mechi ya mkondo wa kwanza Arteta amedai kwamba mchezo huo walipoteza kutokana na vitu vichache vya kimbinu kipindi cha kwanza ambapo wapinzani wao waliwalemea kimbinu zaidi.
“Bado mechi haijaisha ni nusu tu,bado dakika zingine 90 mjini Paris na tunaenda kwa ajili ya kuvuna ushindi hakuna lingine,”Asema Arteta
Kwa mujibu wa mwalimu huyo wanahitaji kuwa katika ubora wao kuangusha Psg kwani wako na timu nzuri ila lengo lao linasalia pale pale kushinda na kufuzu kwenye fainali mwezi wa May 31.
“Ni lazima tuonyeshe uwezo wetu tokea dakika ya kwanza kwamba tunahitaji ushindi huo, nitafanyia mabadiliko ya kimbinu kikosi kabla ya kuelekea Paris na tuko tayari kupindua meza kule.”
Timu hiyo ililazwa goli 1-0 na miamba hao wa ufaransa kupitia goli lake Ousmane Dembele na sasa wanahitaji kushinda kwa zaidi ya magoli 2-0 mechi ya mkondo wa pili ugani Parc De Prince siku ya Jumatano wiki ijayo.
News
Jopo la ushauri na Maimamu eneo la Takaungu lasisitiza Samuel Charo alisilimu kwa hiari yake

Jopo la ushauri na maimamu katika eneo la Takaungu wadi ya mnarani kaunti ya Kilifi limepinga madai yalioibuliwa na wanafamilia wa kijana aliyeuawa baada ya kumuua na kula matumbo ya mzee mmoja aliyekuwa ustadh aliyetambulika kama Ainen.
Kwa mujibu wa ustadh Abubakar Ratili wa masjid Answar kule Takaungu, marehemu Samuel Kirao Charo alisilimishwa na kupewa jina Zakariyah akisisitiza kuwa marehemu alisilimu kwa hiyari yake mbele ya waislam wengine kwenye msikiti huo
Aidha Sheikh Mahadh Ali ambaye pia ni imam wa msikiti Maryam eneo hilo la Takaungu pamoja na Ustadh Mohamed Khamis wameeleza kuwa dini ya kiislam inaruhusu mwili kuzikwa usiku akikashifu swala la kuhusisha hatua hiyo na ushirikina kama ilivyodaiwa na baadhi ya watu.
Jopo hilo pia limeeleza kuwa wanafamilia walihusishwa ila walidinda kushirikiana nao jambo lililopelekea jamii hiyo ya kiislamu kuendeleza maziko ya marehemu kwa mujibu wa Imani ya dini ya kiislam.
News
Wanaharakati na vijana wa Gen -z wazua purukushani kwenye majengo ya bunge la Mombasa
Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu na vijana wa Gen – Z katika kaunti ya Mombasa wemezuiwa kuingia katika bunge la kaunti ya Mombasa kuwasilisha malalamishi yao kuhusiana na bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2025/26.
Vijana hao pamoja na wanaharakati hao waliojawa na hasira wanasema wenyeji wa Mombasa hawajahusishwa kiukamilifu Katika mchakato huo tofauti na inavyofanyika kwenye kaunti zingine nchini.
Wanadai hali ya kutokuwa na uwazi katika utekelezaji wa miswada ya fedha kwenye kaunti hiyo kunachangia kwa shughuli mbalimbali kaunti ya Mombasa kukosa kutekelezwa ipasavyo
Hatahivyo baadae Karani wa bunge la kaunti ya Mombasa salim Juma alipokea malalamishi yao na kuahidi kutoa mwelekeo ufaao Jumanne wiki ijao huku vijana hao wakitishia kurudi tena iwapo malalamishi yao hayatatiliwa maanani.

Bunge la kaunti ya Mombasa/Picha kwa hisani