Connect with us

News

Gataya: Kaunti ya Kilifi Imeonyesha Kuwajibika Kisheria

Published

on

Kamati ya utekelezaji wa sheria katika bunge la Seneti imefanya kikao na Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kutathmini jinsi serikali ya kaunti hiyo inavyoendana na sheria za kitaifa.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mwenda Gataya amesema kati ya kaunti ambazo kamati hiyo imezitembelea, serikali ya kaunti ya Kilifi imeonyesha kuwajibika katika kuzingatia sheria.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho katika makao makuu ya Gavana wa Kilifi, Gataya ambaye pia ni Seneta wa kaunti ya Tharaka Nithi, amesema hatua hiyo imesaidia kuzuia mivutano ya kisheria.

“Tumefurahishwa na kaunti ya Kilifi jinsi ilivyofuata sheria na katiba na kama kamati ya seneti tumeridhia hatua hiyo kwamba kaunti ya Kilifi ni kati ya kaunti bora zaidi kwa kufata sheria na ndio matarajio yetu. Tumeangalia matumizi ya hazina ya wadi pamoja na zengine na kweli ni wazi kwamba imezingatia sheria kwa kuhusisha umma”, Gataya.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema wanalenga kubuni sheria itakayowawezesha wasimamizi wa vijiji kutambulika kisheria, sawa na kubuni sheria itakayojumuisha wananchi katika ujenzi wa shule za Chekechea ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha pamoja na kubuni sheria itakayosimamia bodi ya ukusanyaji ushuru wa kaunti.

Wakati huo huo Gavana Mung’aro amedokeza kwamba tangu achukue hatamu ya uongozi, kaunti ya Kilifi imefaulu kurejesha zaidi ya shilingi bilioni 1.9 kutoka kwa kesi mbalimbali zilizowasilishwa Mahakamani, akisema ni lazima sheria izingatiwe.

“Kuna kesi moja hii kaunti ilikuwa inadaiwa milioni 926 na nikapambana hadi milioni 114, moja ilikuwa bilioni 1.1 na kuenda Mahakamani na tukashinda hiyo kesi na labda wakate rufaa na tupate taarifa kutoka Mahakamani lakini kesi hiyo tulishinda kwa hivyo kaunti imepata bilioni 1.1 pamoja na milioni 800 hiyo ni bilioni 1.9”, Mung’aro.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Aisha Jumwa akosolewa kutokana na matamshi yake

Published

on

Jopo la ushauri la viongozi na maimamu wa Takaungu wadi ya Mnarani kaunti ya Kilifi limeeleza kusikitishwa na kauli zilizotolewa na Aisha Jumwa kuhusiana na tukio la mauaji na maziko ya kijana mmoja eneo hilo lililomtaja kama Zakariyah Kirao Charo.

Likizungumza na vyombo vya habari, jopo hilo likiongozwa na sheikh Mahadh Ali wa msikiti Maryam limemkosoa Jumwa kwa kile lilichosema ameuhujumu uislamu kutokana na kauli alizotoa kwenye mtandao wake wa kijamii wa tiktok kuhusiana na mazishi ya kijana huyo.

Sheikh Mahadh amesema Jumwa alidai kuwa familia ya marehemu haikuhusishwa ilhali walichukua wajibu wa kuihusisha familia kabla ya hatua zozote kuchukuliwa ila wanafamilia wenyewe hawakuonyesha ushirikiano akieleza kuwa jopo hilo pia liligadhabishwa na kauli za Jumwa kuhusiana na namna mchakato mzima wa mazishi ulivyofanywa.

Akiunga mkono kauli hiyo Ustadh Mohamed Khamis amesema kwenye mkao huo kuwa amekuwa akipokea vitisho kutoka kwa Jumwa tangia mtafuruku huo ulipoanza akisisitiza haja ya swala hilo kutotumika kwa namna ya kuchochea wanajamii waislamu na wasio kuwa waislamu katika eneo hilo la Takaungu.

Aisha Jumwa /Picha kwa hisani

Ustadh Mohamed pia amekinzana na kauli kuwa marehemu alisilimishwa akiwa na matatizo ya kiakili akisema ni sharti swala hilo lisiingiziwe siasa.

Continue Reading

News

Viongozi wa Kilifi Wapinga Uekezaji wa Mradi wa Kawi ya Nuklia

Published

on

By

Wizara ya Kawi nchini imefanya kikao cha mazungumzo na uongozi wa kaunti ya Kilifi, pamoja na wabunge na Wasimamizi wa Shirika la NUPEA kuhusu uekezaji wa mradi wa uzalishaji kawi ya Nuklia katika kijiji cha Uyombo wadi ya Matsangoni katika eneo bunge la Kilifi Kazkazini katika kaunti ya Kilifi.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho mjini Kilifi, Waziri wa Kawi nchini Opiyo Wandayi amesema japo viongozi wa kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi hawajaridhishwa na uekezaji wa mradi huo, mazungumzo kuhusu mradi huo bado yataendelea ili kuibuka na mwafaka kwani utasaidia pakubwa katika uzalishaji kawi.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema msimamo wa serikali ya kaunti ya Kilifi pamoja na wananchi bado uko pale pale wa kuendelea kupinga uekezaji wa mradi huo wa mabilioni ya pesa, akisema utafiti uliofanywa umebaini kwamba mradi huo unaathari kubwa kwa wananchi.

Hata hivyo Mbunge wa Kilifi Kazkazini Owen Baya amesema kama viongozi kutoka kaunti ya Kilifi hawako tayari kupokea mradi huo wa uzalishaji kawi ya Nuklia, akisema changamoto nyingi bado hazitatuliwa katika mradi huo ambazo ni athari kwa wananchi.

Kikao hicho hata hivyo kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Malindi Amina Mnyazi, Mbunge wa Kaloleni Paul Katana, Mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, Mbunge wa Ganze Kenneth Tungule, Katibu katika Wizara ya masuala ya vijana na michezo nchini Fikirini Jacobs miongoni mwa viongozi wengine.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.