Connect with us

News

Liverpool Mabingwa Mara 20 Epl

Published

on

Sasa Ni rasmi kwamba kilabu ya Livrpool ndiyo mabingwa wa Ligi kuu Uingereza baada ya kuvuna ushindi mnono wa magoli 5-1 dhidi ya Tottenham Hotspurs Ugani Anfield.

Mshambulizi Dominik Solanke aliwaweka uongozini dakika ya 12 kabila ya mshambulizi Luis Diaz kuisawazishia vijana wa kocha Arne Slot kunako dakika ya 16. Kiungo Alexis Mc Allister aliweka kambani chuma ya pili dakika 24 kabila ya winga Cody Gakpo kuweka goli la tatu dakika ya 34.

Goli la nne lilitiwa kimyani na mshmabulizi nyota Mohammed Salah dakika ya 63. Huku Goli la Tano likitiwa nyavuni kwa kujifunga kutoka kwa beki wa Spurs Destiney Odogie.

Ushindi huu ukiipa The Reds alama 82 kileleni baada ya mechi 34 huku kilabu ya Arsenal ikifuata nafasi ya pili na alama 67 nao Newcastle United ikiwa ni ya tatu na alama 62 ,mancity ni ya nne na alama 61 Huku Chelsea akifunga tano bora na alama 60

Vilabu vya Southampton,Leicester city na Ipswich Town vyote vikishushwa ngazi ligi hio navyo Leeds United na Burnley tayari zimejikatia tiketi ya kurejea Epl baada ya kuongoza ligi ya Championship na alama 84.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kadinali Bacciu Atangaza Kutohudhuria Kikao cha Conclave

Published

on

By

Kadinali Giovanni Angela Bacciu ametangaza kujiondoa katika kikao cha siri cha kumchagua Papa mpya kilichopangwa na Ofisi ya Vatican kuanza rasmi mwezi Mei 7.

Katika taarifa yake aliyoitoa kupitia Wakili wak siku ya Jumanne tarehe 29, Kadinali Bacciu amesema ameamua kutii wasia ulioweka wa Hayati Papa Francis  ingawa alidumisha kutokuwa na hatia.

“Kwa kuwa moyoni mwangu nina wema wa Kanisa ambalo nimelitumikia na nitaendelea kulitumikia kwa uamunifu na upendo na kuchangia ushirika na utulivu wa Conclave, nimeamua kutii kama nilivyofanya siku zote wakati wa Papa Francis na nitasalia kuamini kwamba sina hatia”, alisema Kadinali Bacciu.

Kadinali Bacciu mwenye umri wa miaka 78 na mzaliwa wa taifa la Italia amegongwa vichwa vya habari kutokana na msimamo wake huku baadhi ya wachanguzi wakisema uamuzi wake umetokana na sintofahamu zilizokuwepo kati yake na Hayati Papa Francis mwaka wa 2020 baada ya kuagizwa na Papa Francis kujiuzulu kwa kupatikana na kashfa ya ufisadi.

Continue Reading

News

Mbogo: Kaunti ya Mombasa Imeshindwa Kutatua Mzozo wa Ardhi

Published

on

By

Aliyekuwa mbunge wa Kisauni Ali Mbogo ameikosoa serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kushindwa kutatua suala tata la uskwota linalowakumba wakaazi wengi wa kaunti hiyo.

Akizungumza katika eneo la Kisauni katika kaunti ya Mombasa, Mbogo amesema tatizo la uskwota limeendelea kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya ardhi na ukosefu wa usalama katika maeneo mengi ya kaunti ya Mombasa huku serikali ya kaunti hiyo ikionekana kulifumbia macho suala hilo.

Mbogo amedai kwamba maelfu ya wakaazi wa Kisauni na Mombasa kwa jumla wanaishi kwa hofu ya kufurushwa katika ardhi zao walizoishi tangu jadi kufuatia ukosefu wa hati miliki.

Wakati huo huo amedokeza kwamba baadhi ya maafisa wa serikali ya kaunti hiyo wanahusishwa na visa vya uporaji wa ardhi za umma kwa kushirikiana na waekezaji jambo ambalo amelitaja kuwa dhulma.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.