Connect with us

News

Nuno: Usalama umeimarishwa msimu wa Pasaka

Published

on

Kamanda wa Polisi kanda ya Pwani Ali Nuno amesema usalama umeimarishwa msimu huu wa sherehe za Sikukuu ya Pasaka huku akiwataka wakaazi pamoja na wageni wa wanaolenga kuzuru kanda ya Pwani kutokuwa na hofu.

Nuno amewahimiza abiria wa magari ya uchunguzi wa umma kuhakikisha madereva wanazingatia sheria za barabarani ili kudhibiti ajali za mara kwa mara.

Aidha amesema ajali nyingi ambazo zimekuwa zikifanyika zimekuwa zikisababishwa na madereva wasiokuwa waangalifu barabarani huku wengine wakiwa walevi, wachovu miongoni mwa tabia zingine zisizofaa.

Vilevile, ameyaonya magenge ya kihalifu katika kaunti za Kwale na Mombasa ambayo yamekuwa yakiwahangaisha wenyeji kwamba yatakabiliwa kisheria.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.