Connect with us

News

Fikirini, Ameapishwa Rasmi kuwa Katibu katika Wizara ya Michezo na Vijana

Published

on

Rais William Ruto ameshuhudia kuapishwa kwa mawaziri wawili wapya pamoja na makatibu katika Wizara mbalimbali nchini katika halfa iliyoandaliwa katika Ikulu ya Nairobi.

Wakati wa halfa hiyo, mawaziri na makatibu hao wameapa kuwajibikia majukumu yao kikamilifu kwa kuzingatia kanuni za nchi sawa na kuheshimu muongozo wa Katiba.

Geoffrey Ruku aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Utumishi wa umma nchini pamoja na Hanna Cheptumo kama Waziri wa jinsia wameapishwa rasmi kuanza majukumu yao ya kikazi.

Wengine walioapishwa ni makatibu katika Wizara mbalimbali baada ya kuidhinishwa na bunge la kitaifa ambapo Fikirini Jacobs kama Katibu katika Wizara ya Michezo na vijana, Caren Achieng Ageng’o, Aden Abdi Mila miongoni wa wengine wameahidi kutumikia taifa kikamilifu.

Akizungumza baada ya kuapishwa kwa mawaziri na makatibu hao, Rais William Ruto amewashauri mawaziri na makatibu hao kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamalifu ili kufanikisha malengo ya wananchi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kadinali Bacciu Atangaza Kutohudhuria Kikao cha Conclave

Published

on

By

Kadinali Giovanni Angela Bacciu ametangaza kujiondoa katika kikao cha siri cha kumchagua Papa mpya kilichopangwa na Ofisi ya Vatican kuanza rasmi mwezi Mei 7.

Katika taarifa yake aliyoitoa kupitia Wakili wak siku ya Jumanne tarehe 29, Kadinali Bacciu amesema ameamua kutii wasia ulioweka wa Hayati Papa Francis  ingawa alidumisha kutokuwa na hatia.

“Kwa kuwa moyoni mwangu nina wema wa Kanisa ambalo nimelitumikia na nitaendelea kulitumikia kwa uamunifu na upendo na kuchangia ushirika na utulivu wa Conclave, nimeamua kutii kama nilivyofanya siku zote wakati wa Papa Francis na nitasalia kuamini kwamba sina hatia”, alisema Kadinali Bacciu.

Kadinali Bacciu mwenye umri wa miaka 78 na mzaliwa wa taifa la Italia amegongwa vichwa vya habari kutokana na msimamo wake huku baadhi ya wachanguzi wakisema uamuzi wake umetokana na sintofahamu zilizokuwepo kati yake na Hayati Papa Francis mwaka wa 2020 baada ya kuagizwa na Papa Francis kujiuzulu kwa kupatikana na kashfa ya ufisadi.

Continue Reading

News

Mbogo: Kaunti ya Mombasa Imeshindwa Kutatua Mzozo wa Ardhi

Published

on

By

Aliyekuwa mbunge wa Kisauni Ali Mbogo ameikosoa serikali ya kaunti ya Mombasa kwa kushindwa kutatua suala tata la uskwota linalowakumba wakaazi wengi wa kaunti hiyo.

Akizungumza katika eneo la Kisauni katika kaunti ya Mombasa, Mbogo amesema tatizo la uskwota limeendelea kuwa chanzo kikuu cha migogoro ya ardhi na ukosefu wa usalama katika maeneo mengi ya kaunti ya Mombasa huku serikali ya kaunti hiyo ikionekana kulifumbia macho suala hilo.

Mbogo amedai kwamba maelfu ya wakaazi wa Kisauni na Mombasa kwa jumla wanaishi kwa hofu ya kufurushwa katika ardhi zao walizoishi tangu jadi kufuatia ukosefu wa hati miliki.

Wakati huo huo amedokeza kwamba baadhi ya maafisa wa serikali ya kaunti hiyo wanahusishwa na visa vya uporaji wa ardhi za umma kwa kushirikiana na waekezaji jambo ambalo amelitaja kuwa dhulma.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.