Connect with us

News

Maadhimisho ya Jumapili ya Matawi

Published

on

Waumini wa madhehebu mbalimbali ya kikristu wamemiminika makanisani kuadhimisha Jumapili ya matawi, juma moja kabla ya maadhimisho ya sikukuu ya Pasaka.

Waumini wa madhehebu ya Anglikana, Orthodox na Lutheran miongoni mwa madhehebu mengine yanaadhimisha Jumapili ya matawi kukumbuka jinsi Yesu Kristu mwana wa Mungu alivyoingia katika mji Yerusalemu, akiwa amepanda punda ishara ya unyenyekevu na amani.

Kulingana na Imani ya dini ya kikristu maadhimisho haya yanaashiria jinsi watu wa Israeli hasa Wayahudi, walivyompokea Yesu Kristu kwa shangwe, wakipeperusha matawi ya mitende na kumtandikia mavazi njiani, wakisema, “Hosana Hosana! Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana!”
Matawi ya mitende ndiyo asili ya jina la siku hii “Jumapili ya Matawi,” ambapo Jumapili ya matawi huashiria mwanzo wa juma kuu; yani wiki ya mwisho ya maisha ya Yesu Kristu kabla ya kuteswa, kufa na kufufuka ambapo waumini wa dini ya kikristu hukamilisha juma hilo na sikukuu ya Pasaka.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.