Connect with us

News

Murkomen: Serikali Kuajiri Maafisa wa Polisi elfu 10

Published

on

Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen amesema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha inaajiri maafisa wa Polisi elfu 10 katika kipindi cha miezi miwili ijayo.

Akizungumza mjini Kilifi wakati wa ziara yake ya kutathmini maswala ya kiusalama katika ukanda wa Pwani, Waziri Murkomen amesema hatua hiyo itasaidia kuimarisha usalama mashinani.

Murkomen amesema taifa la Kenya limeshuhudia changamoto nyingi za kiusalama kutokana na idadi ndogo ya maafisa wa usalama nchini, akisema juhudi zilizowekwa na serikali zitasaidia kuimarisha usalama kote nchini.

Waziri huyo wa usalama hata hivyo amedokeza kwamba tayari serikali inaendelea na mpango wa kununua magari ya maafisa wa usalama elfu tano ambayo yatasambazwa kwa vitengo mbalimbali vya kiusalama ili kusaidia kuimarisha usalama mashinani.

Kauli yake imejiri baada ya wananchi kulalamika kuhangaishwa na magenge ya kihalifu huku maafisa wa usalama wakishindwa kutekeleza majukumu yao kufuatia idadi ndogo ya maafisa wa usalama sawa na uhaba wa magari ya Polisi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.