News
Mwadime: Visa vya Wakenya Kuteswa Nchini Saudia Vimepungua

Katibu katika Wizara ya Leba nchini Shadrack Mwadime amesema visa vya wakenya kuteswa na kuuwawa katika mataifa ya ughaibuni hasa nchini Saudia Arabia vimepungua pakubwa.
Mwadime amesema kupungua kwa visa hivyo kumetokana na serikali kuchukua hatua hitajika za kutia saini mkataba wa makubaliano ya kazi baina ya nchi hizi mbili.
Mwadime amesema serikali ya Kenya inaendeleza mazungumzo na serikali ya Saudia ili kufanikisha mkataba huo na kuwawezesha wananchi kuwa huru pindi wanapopata ajira katika taifa hilo.
Katibu huyo amesema shughuli hiyo itakapofanikishwa ni wazi kwamba visa vya wakenya kuuwawa na kuteswa nchini Saudia vitasitishwa kabisa.
Wakati huo huo amewashauri wakenya kutembelea ubalozi wa Kenya ili kufahamisha ubalozi huo kuhusu kazi wanazoenda kuzifanya na kushauriwa zaidi kuhusu mwongozo wa jinsi watakavyoripoti visa vya unyanyasaji.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.