Connect with us

News

Mshukiwa wa Ugaidi Azuiliwa na Polisi Mombasa

Published

on

Maafisa wa Polisi mjini Mombasa wanamzuilia mwanamme mmoja baada ya kupatikana akiwa amebeba risasi na bidhaa zengine zinazokisiwa kuwa vilipuzi katika kivuko cha Feri cha Likoni.

Maafisa wa Polisi wamesema jamaa huyo anayefahamika kwa jina Shinali Amuna Komoro amekamatwa alipokuwa akivuka kivuko cha Feri cha Likoni akitokea kisiwani Mombasa.

Maafisa hao wamesema kabla ya mshukiwa huyo kukamatwa alikuwa ameabiri basi lililokuwa likivuka feri kuelekea upande wa Likoni na ametiwa nguvuni wakati maafisa wa usalama walipokuwa wakifanya ukaguzi katika kivuko hicho.

Akithibitisha kukamatwa kwake, Kamanda wa Polisi eneo la Likoni Geoffrey Ruheni amesema huenda mshukiwa alikuwa amepanga njama ya kutekeleza mashambulizi ya kigaidi ndani ya Feri.

Ruheni amesema mshukiwa huyo amekabidhiwa maafisa wa kupambana na ugaidi nchini ATPU kwa uchunguzi zaidi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Published

on

By

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.

Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.

Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.

Continue Reading

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.