Connect with us

News

Muturi, Amshutumu Rais Ruto Baada ya Kutimuliwa Kazini

Published

on

Aliyekuwa Waziri wa Utumishi wa umma nchini Justin Muturi amejitokeza na kupinga kauli ya Rais William Ruto aliyoitoa siku chache zilizopita kwamba alifutwa kazi kwa misingi ya kutowajibika kazini.

Muturi amesema kutimuliwa kwake kazini kulichangiwa na msimamo wake wa kuishinikiza serikali kupitia Rais  Ruto kukomesha visa vya utekaji nyara na mauaji ya kiholela nchini.

Katika kikao na Wanahabari jijini Nairobi, Muturi amesema hajutii kufutwa kwake kazi, akisema madai yaliyoibuliwa na Rais kwamba alikuwa haudhurii vikao vya baraza la mawaziri ni uongo mtupu kwani alikuwa amewasilisha maombi rasmi ya kutohudhuria vikao vya baraza la mawaziri.

Muturi amesema licha ya kushinikiza swala la utekaji nyara na mauaji ya kiholela nchini kukomeshwa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa na idara husika bali tabia hiyo imekuwa ikiendelea, jambo ambalo sio mikakati ya ajenda ya Kenya kwanza.

Wakati huo huo amemshtumu rais Ruto akisema amekuwa akijitokeza hadharani na kutoa kauli za uongo kuhusu mikakati ya serikali ilhali hakuna mipango yoyote serikali ambayo rais Ruto anatekeleza.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Published

on

By

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.

Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.

Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.

Continue Reading

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.