News
Mhubiri tata Kipngeny Ametiwa Nguvuni Eneo la Chonyi

Maafisa wa Idara ya upelelezi nchini DCI wamemtia nguvuni Mhubiri tata Julius Kimtai Kipngeny wa Kanisa la Mlango wa Miujiza Deliverance katika eneo la Mishomoroni kaunti ya Mombasa.
Kulingana na maafisa hao, Mhubiri huyo amekamatwa akiwa na mifupa na vitu vingine vya maajabu akiwa katika kijiji cha Chonyi kaunti ya Kilifi pamoja na mwandani wake Baraka Tsuma mwenye umri wa miaka 32.
Maafisa hao wamesema Kipngeny na Tsuma walikuwa wakiendeleza ibada na kundi la wanawake kwenye ghofu la jumba hali ambayo iliwatia hofu maafisa hao.
Akithibitisha kutiwa nguvuni kwa Mhubiri huyo tata, Afisa wa Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI kaunti ya Kilifi David Siele amesema mifupa hiyo imepelekwa kwa uchunguzi wa kitaalam ili kuthibitisha iwapo ni mifupa ya binadamu au la.
Hata hivyo imebainika kwamba washirika wa Kanisa hilo ambalo anaongoza Mhuburi huyo tata ni wa jinsia ya kike pekee.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.