News
Nassir, Awaonya Vijana Wanaojihusisha na Uhalifu Mombasa

Gavana wa kaunti ya Mombasa Abdulswamad Shariff Nassir amekashifu vikali ongezeko la vijana wadogo wanaoendeleza uhalifu katika kaunti hiyo.
Abdulswamad amewakosoa wale wanaosema kuwa vijana hao wanatekeleza uhalifu kutokana na ukosefu wa ajira, akisema wengi wa vijana hao ni wa umri mdogo.
Aidha amekariri kuwa vijana walio chini ya umri wa miaka 18 hawawezi kupewa ajira, akisema ni sharti wazazi wawajibike katika malezi ya watoto wao ili kuwaepusha dhidi ya utovu wa maadili.
Kauli yake imeungwa mkono na Mwenyekiti wa baraza la kitaifa la ushauri kwa waislamu KEMNAC, Sheikh Juma Ngao ambaye amesema wazazi wengi wamezembea katika kuwalea watoto wao hali inayowasababishia vijana hao kujiingiza katika uhalifu.
Sheikh Ngao amependekeza vijana hao wakamatwe na wachukuliwe hatua kali za kisheria pasi na kujali umri wao.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.