News
Spika Mwambire Alalamikia Kucheleweshwa kwa Fedha za Kaunti

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amelalamikia hatua ya serikali kuu kuchelewesha usambazaji wa fedha za serikali za kaunti, akidai kwamba hatua hiyo imelemaza utendakazi mashinani.
Mwambire amesema hali hiyo huenda ikachangia idadi ya wafanyakazi ikiwemo maafisa wa mabunge ya kaunti sawa na viongozi wa mabunge hayo kupunguzwa.Aidha amesema licha ya changamoto hiyo, wafanyakazi wa bunge la kaunti ya Kilifi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa bidii kwa lengo la kuboresha gatuzi la Kilifi.
Wakati huo huo amesifia bunge la kaunti ya Kilifi akilitaja kama bunge bora zaidi kwani halijahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma jinsi inavyoshuhudiwa katika mabunge mengine ya kaunti humu nchini.
Kiongozi huyo hata hivyo amesema hali hiyo inadhihirisha wazi kwamba viongozi ndani ya bunge hilo wanalenga zaidi matakwa ya wananchi na wala sio kujinufaisha binafsi.
News
Ruku: Serikali kuajiri vijana laki moja kwa NYS

Serikali inalenga kuajiri zaidi ya vijana laki moja katika Shirika la huduma kwa vijana wa taifa NYS.
Waziri wa utumishi wa umma nchini Geoffrey Ruku amesema hatua hiyo itachangia kuboreshwa kwa huduma za umma sawa na kuhakikisha Shirika la NYS linakuwa nguzo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Akizungumza katika kaunti ya Machakos, Waziri Ruku amesema hatua hiyo itapunguza utegemeaji wa ufadhili wa umma kwani shirika hilo itapanua mikakati bora ya serikali ya kibiashara pamoja na kufanikisha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Waziri Ruku amelishinikiza bunge la kitaifa kuharakisha marekebisho ya mswada wa NYS ambao utawalishwa na Wizara yake bungeni ili kusawazisha mfumo wa kisheria wa shirika hilo.
Wakati huo huo amewataka vijana kukumbatia mipango ya serikali ya kujumuisha wananchi wote pamoja katika kufanikisha ajenda ya serikali ya maendeleo endelevu hadi mashinani.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.