News
Spika Mwambire Alalamikia Kucheleweshwa kwa Fedha za Kaunti

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire amelalamikia hatua ya serikali kuu kuchelewesha usambazaji wa fedha za serikali za kaunti, akidai kwamba hatua hiyo imelemaza utendakazi mashinani.
Mwambire amesema hali hiyo huenda ikachangia idadi ya wafanyakazi ikiwemo maafisa wa mabunge ya kaunti sawa na viongozi wa mabunge hayo kupunguzwa.Aidha amesema licha ya changamoto hiyo, wafanyakazi wa bunge la kaunti ya Kilifi wamekuwa wakitekeleza majukumu yao kwa bidii kwa lengo la kuboresha gatuzi la Kilifi.
Wakati huo huo amesifia bunge la kaunti ya Kilifi akilitaja kama bunge bora zaidi kwani halijahusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma jinsi inavyoshuhudiwa katika mabunge mengine ya kaunti humu nchini.
Kiongozi huyo hata hivyo amesema hali hiyo inadhihirisha wazi kwamba viongozi ndani ya bunge hilo wanalenga zaidi matakwa ya wananchi na wala sio kujinufaisha binafsi.
News
Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.
Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.
Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.
News
Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.
Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.
Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.
Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.
Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.