Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa Walalamikia Ukosefu wa Maji Kwenye Soko Hilo

Published

on

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa kaunti ya Kilifi wamelalamikia ukosefu wa maji kwenye Soko hilo ambapo wafanyibiashara wengi wanalitegemea kuendeleza shughuli zao za kila siku.

Kulingana na mwenyekiti wa Soko hilo Millicent Mbodze ukosefu wa maji katika soko hilo limeathiri biashara zao kwani maji yanatumiwa kuonsha bishaa nyingi kama vile matunda, mboga na hata samaki kwa wanaouza samaki katika soko hilo.

Aidha amesema wateja wengi wanalalamikia hali mbaya ya ya soko hilo kwani kumejaa uchafu kila mahali hali inayowasababishia kuhofia afya yao.

Amesema tayari wateja wengi wanasusia maeneo hayo jambo ambalo liewasababishishia hasara kubwa kwani bidhaa nyingi huozea sokoni.

Wakati huo huo Mbodze amesema licha ya kuwasilisha swala hilo kwa kwa wahusika sawa na serikali ya kaunti ya Kilifi,bado halijatatuliwa.

Anasema imekuwa changamoto kwa wafanyabiashara kwani imekuwa shida kutumia hata sehemu za kujisaidia sokoni humo huku ikiwalazimu kutafuta bidhaa hiyo kwenye kituo kimoja cha mafuta kilichoko eneo hilo.

Huku hayo yakijiri benki ya dunia imetenga shilingi bilioni 2.58 kuimarisha mpango wa usabasazaji maji katika kaunti ya kilifi.

Mradi huo unalenga miji ya malindi , kilifi na mtwapa na utahusisha kubadilishwa kwa mabomba makuku ya maji na kuweka mabomba mapya.

Ikumbukwe Gavana wa kilifi Gedion Mung’aro alisema miradi hiyo itahakikisha kuwa kaunti hiyo iko na maji safi na yakutosha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyibiashara Malindi Waelezea Kudorora Kwa Utalii Kutokana na Hoteli Kufungwa Eneo Hilo

Published

on

Wafanyibiashara katika sekta ya utalii mjini Malindi kaunti ya Kilifi wameelezea kudorora kwa sekta hiyo kutokana na hatua ya mahoteli mengi eneo hilo kufungwa.

Wakizumguza na vyombo vya habari wafanyiabisha hao wakiongozwa na Boniface Mutuku, wamesema kuwa kufungwa kwa mahoteli kumewasababishia kukadiria hasara kwani kuna bidhaa nyingi ambazo hutumiwa na watalii sasa hivi zinaendelea kuharibika.

Kulingana hali hiyo imesababisha kupungua kwa kiwango kikubwa cha watalii ambao walikuwa wakizuru mji huo hapo awali hivyo kuathiri biashara zao.

Mutuku amemuomba gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kubuni mbinu za kufufua mahoteli yaliyosambaratika mjini Malindi ambayo yalikua kivutio kikubwa cha utalii eneo hilo ili kuboresha maisha yao.

Aidha ameongeza kuwa kupitia uboreshaji wa maeneo ya utalii na mahoteli nafasi za ajira zitaongezeka na kuboresha maisha ya wakaazi wa eneo hilo na kenya mzima kwa ujumla.

Kwa upande wake Anthony Muasya ambaye pia ni mmoja wa wafanyibiashara hao amewanyoshea kidole cha lawama baadhi ya viongozi mjini Malindi kwa kile anachodai kuwa wameshindwa kuwajibikia suala la kuboresha sekta ya utalii na pia viwanda.

Kulinanga na Muasya viongozi wako na uwezo wa kuboresha utalii na viwanda lakini kufikia sasa hakuna jambo lolote ambalo limefanyika kufikia sasa.

Amewataka viongozi hao kuwajibika ili kuhakikisha kuwa viwanda hivyo vinaimarika ili kuimarisha biashara zao.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.