Connect with us

News

Lazima Tufunge Tunisia Magoli ya Mapema, Kauli ya Kocha Odemba Kuelekea Mechi ya Starlets

Published

on

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee starlets Beldine Odemba ana amini kwamba uwepo wa mashabiki katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex Ijumaa hii itawapa msukumo timu hiyo wanapojianda kwa mechi ya kufuzu dimba la Afrika AWCON mwakani.

Akizungumza na wanahabari Odemba amesema anasubiri mchezaji wa mwisho kambini Jumatano hii.

“Tuko na karibu full house baada kuwasili kwa wachezaji zaidi ya kumi wa kulipwa,Tunasubiri mchezaji wa mwisho Jumatano hii.” Kocha anazidi kuelezea kwamba, “Lengo letu ni kushinda Tunisia hapa Nyumbani kabla ya mechi ya mkondo wa pili mjini Tunisia Feb 26. Kwa mujibu wa mwalimu huyo na kikosi mchanganyiko Yani chipukizi na wazoefu inampa msukumo kwamba tutaandikisha matokeo chanya, “Wachezaji chipukizi ndio Harambee starlets ya badaye kuwepo kwao kambini inanisaidia kuwa na upana wa kikosi na kujenga kikosi Cha usoni vile vile.Kwa upende wake kiungo wa Besikitas ya Uturuki Cynthia Shilwatso ni kwamba hawataki kujuta Tena baada ya kubanduliwa na Botswana mwaka Jana,” Lengo Letu ni kushinda nyumbani ndio tuenjoy mchezo ugenini, Ni lazima tufunge Tunisia magoli ya mapema kilichotupata mwaka Jana kisitupate tena.”

Kambi ya Harambee starlets imekamilika baada ya wachezaji wa kigeni wote kuwasili kwa pambano la kufuzu dimba la AWCON dhidi ya Tunisia Ijumaa hii ugani Ulinzi Sports Complex mjini Nairobi.

Mechi hiyo itapigwa majira ya saa tisa kiingilio ni shs. 100 mashabiki wa kawaida na shs. 500 watu mashuhuri (VIP).

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Nyakang’o, apendekeza mgao wa shilingi bilioni 1.6

Published

on

By

Mdhibiti wa bajeti nchin Margaret Nyakang’o amependekeza kuongezwa kwa kiwango cha bajeti ya ofisi yake kutoka shilingi milioni 7.2 hadi shilingi bilioni 1.6 ili kufanikisha majukumu yake.

Akizunguza mjini Mombasa wakati wa kikao na kamati ya uekezaji wa umma na hazina maalum katika bunge la Seneti, Nyakang’o amesema bajeti hiyo ya ofisi yake iko chini mno katika kufanikisha mikakati endelevu ya majukumu yake ya kikazi.

Hata hivyo amesema iwapo bajeti hiyo itaongezwa ofisi yake itakuwa na wakati mwafaka wa kukagua miradi ya maendeleo katika kaunti zote nchini.

Continue Reading

News

Gavana Mung’aro afanya kikao na Gach Group kuhusu uekezaji wa Madini

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro amefanya kikao cha mazungumzo na waekezaji kutoka Kampuni ya Gach Group kuhusu uekezaji wa madini katika eneo la Magarini utakavyochangia pato la kaunti.

Kulingana na Gavana Mung’aro, uwekezaji huo utafungua nafasi za ajira kwa zaidi ya watu 500 wa eneo bunge la Magarini na kaunti ya Kilifi kwa jumla kwani waekezaji hao wanalenga madini ya Titanium na lime.

Gavana Mung’aro ameweka wazi kwamba serikali yake imejitolea kuweka mazingira bora kwa waekezaji sawa na kufanikisha mpango endelevu wa kibiashara utakaowanufaisha wenyeji.

Akizungumza baada ya kukutana na waekezaji hao kutoka taifa la Gambia, Gavana Mung’aro amedokeza kwamba kaunti ya Kilifi iko tayari kushirikiana na waekezaji wenye malengo bora kwa wananchi ili kufanikisha maendeleo.

Hata hivyo viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Mwenyekiti wa Gach Group Dkt Abubakar Jawara, aliyekuwa Mbunge wa Magarini Harrison Kombe, aliyekuwa Seneta wa Samburu Sammy Leshore pamoja na viongozi wengine wa kaunti.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.