Connect with us

National News

Ufisadi Humu Nchini Umekuwa Tatizo, Koome Asema

Published

on

Photo: Courtesy

Jaji mkuu nchini Martha Koome ameelezea kutamaushwa na ufisadi ambao bado umekithiri katika idara mbalimbali za umma, akisema ufisadi humu nchini umekuwa tatizo la kitaifa ambalo limeathiri maendeleo.

Akizungumza jmjini Mombasa wakati wa kongamano la baraza la kitaifa kuhusu utawala na haki, Jaji Koome amesema idara za haki zina jukumu kubwa la kuzuia, kuchunguza, kulinda, kusikiliza na kutoa hukumu katika kesi za ufisadi.

Jaji Koome, amesema idara ya Mahakama nchini imeanzisha mchakato wa kubuni sera za kupambana na ufisadi zitakazokamilika na kuzinduliwa rasmi mwezi Machi mwaka huu, na kwamba mapambano dhidi ya rushwa na uhalifu wa kiuchumi ni jukumu la kila mmoja.

Wakati uo huo amesema wataimarisha ushirikiano, uwezo, kuboresha mfumo wa kisheria, sera na utawala, kuimarisha ufanisi na uwajibikaji katika vita dhidi ya ufisadi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.