Connect with us

National News

Ruto Aomboleza Kifo cha Seneta wa Baringo

Published

on

Photo: Shutterstock

Viongozi mbalimbali nchini watuma rasila zao za rambirambi kwa familia ya mwendazake Seneta wa Baringo William Cheptumo, aliyeaga dunia baada ya kuugua kwa mda mfupi katika hospitali ya Nairobi.

Wakiongozwa na rais William Ruto, viongozi hao wamemtaja mwendazake kama kiongozi mwenye maendeleo na aliyejitolea kama mtumishi wa umma kuwafanyia wananchi wake maendeleo.

Rais Ruto amemtaja mwendakazi kama kiongozi mchapa kazi huku akisema wakaazi wa kaunti ya Baringo wamepata piga kubwa kwa kuondokewa na kiongozi wao.

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Seneti Amason Jeffah Kingi, amesema bunge la seneti limepata pigo baada ya kumpoteza kiongozi mchapa kazi ambaye alikuwa mstari wa mbele katika kuchangia hoja muhimu bungeni.

Cheptumo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 57 baada ya kuugua kwa mda mfupi wakati akipokea matibabu katika hospitali ya Nairobi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Chonga: Wakenya Wanaosafiri Ughaibuni Kusaka Ajira Hawazingatii Sheria za Leba

Published

on

By

Mwenyekiti wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa Ken Chonga amesema baadhi ya wakenya ambao wanasafiri katika mataifa ya miliki za kiarabu kusaka ajira wamekosa kuzingatia sheria za Wizara ya Leba nchini na kuangukia mikononi mwa walaghai.

Chonga amesema ni lazima wakenya hao wachunguze mawakala wanaowasafirisha katika mataifa hayo kama wanatambulika na serikali, ndipo waingie katika mikataba ya uajiri ambayo imezingatia sheria za Leba nchini.

Akizungumza na Wanahabari mjini Kilifi, Chonga ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kusini amesema ili wakenya waepuke madhila mbalimbali kutoka kwa waajiri wao katika mataifa hayo ni lazima wasafirishwe na mawakala waliosajiliwa na serikali.

Wakati huo huo amesema japo serikali iko mbioni kuhakikisha inawatafutia wakenya kazi katika mataifa ya ughaibuni ni lazima wanaosaka ajira za ughaibuni waingie katika mkataba wa uajiri kabla ya kusafiri nje ya nchi.

Continue Reading

National News

Chibule: Visa vya Dhulma za Kijinsi Vimepungua Kilifi

Published

on

Serikali ya kaunti ya Kilifi imesema visa vya dhulma za kijinsia katika kaunti hiyo vimepungua kwa kiwango kikubwa.

Kulingana na Naibu Gavana wa kaunti hiyo Flora Mbetsa Chibule, visa hivyo viliongezeka zaidi msimu wa maambukizi ya virusi vya Corona, ambapo kaunti ya Kilifi iliorodheswa nafasi ya tatu nchini baada ya kaunti ya Bungoma na Samburu.

Chibule amesema kwa sasa ni asilimia 12.3 pekee ya visa hivyo vilivyoripotiwa tofauti na asilimia 30 wakati wa maambukizi ya Corona, akisisitiza kwamba juhudi hizo zimefanikiwa kupitia ushirikiano wa jamii na wadau mbalimbali.

Kiongozi huyo amedokeza kwamba serikali ya kaunti imetoa mafunzo kwa maafisa wa kutoa ushauri nasaha ili kusaidia kupambana na visa hivyo mashinani, akisema juhudi hizo zitaendelezwa sawa na kudhibiti madhila hayo.

Wakati uo huo ameweka wazi kwamba kaunti hiyo imekamilisha ujenzi wa sehemu salama ya kuwahifadhi watoto wanaopitia dhulma za kijinsia wakati kesi zao zikiendelea Mahakamani.

Continue Reading

Trending

Copyright © 2024 Coco Media.