National News
Washukuwa Wawili wa Kundi la Kigaidi la Alshabab Watiwa Nguvuni

Watu wawili wanaoshukuwa kuwa wanamgambo wa kundi la kigaidi la Alshabab wametiwa nguvuni na maafisa wa kupambana na magaidi nchini ATPU katika kaunti ya Mandera.
Kulingana na maafisa hao, mshukiwa mmoja alifaulu kuvuka mpakani kutoka El-Adde nchini Somalia hadi nchini Kenya na kufanikiwa kupata kitambulisho cha kitaifa ili kutimiza malengo ya kigaidi.
Idara ya upelelezi wa jinai nchini DCI imesema washukiwa hao wawili akiwemo Issac Mohammed Abdi na Noor Yakub Ali wote wakiwa na umri wa miaka 29, walikuwa wamepanga kuwateka nyara raia wa China waliokuwa wakitengeza mabomba ya maji katika uwanja wa ndege wa Mandera.
DCI imesema Mohammed alikuwa amepanga njama na mwandani wake humu nchini kumsaidia kumteka nyara raia wa China kwa gharama ya shilingi elfu laki moja ili kufanikisha mipango ya kusafirisha raia wa China hadi Somalia.
Maafisa hao wamesema baadaye walibaini kwamba gaidi mwengine Noor Yakub Ali, alikuwa amepanga kusaidia usafirisha wa utekaji nyara kwa gharama ya shilingi laki tatu hadi eneo la El-Adde nchini Somalia kabla ya njama hiyo kutibuka.
Washukiwa hao wanaendelea kuzuiliwa na maafisa wa kupambana na magaidi nchini ATPU kwa uchunguzi zaidi.
National News
Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).
Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa
Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.
Taarifa Ya Elizabeth Mwende
National News
Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.
Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.
Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.
Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.
Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.
Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.
Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.
Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.
Taarifa ya Joseph Jira
-
Entertainment9 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment21 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News18 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni