Connect with us

Business

Wakulima Tanariver waeleza matumaini ya mazao bora

Published

on

Wakulima katika mradi wa unyunyizaji maji mashamba katika mradi wa Hola irrigation Scheme Kaunti ya Tanariver wameeleza matumaini ya kupata mazoa bora kufuatia hatua ya serikali kubadili mfumo wa mitambo ya usambazaji maji.

Walisema mitambo ya jereneta iliyokuwa ikitumia mafuta ilikuwa na gharama ila kwa sasa hatua ya serikali kuekeza katika mpango wa umeme utachangia faida zaidi.

Kulingana na Maurice Adero na Ernest Akumu changamoto ya maji vile vile utumizi wa mafuta kuendesha mitambo ya usambazaji maji vilichangia wakulima kupata hasara.

“Hapo nyuma kilimo chetu kilikuwa na shida kidogo mambo ya maji kwa sababu ilikuwa unapopanda mimea huwezi vuna kabla hujapata tatizo la kukosa maji, sasa tumetoka kwa donda sugu la mambo ya dizeli, kitambo dizeli inunuliwe mpaka ifike Tanariver pengine ipelekwe kwa vituo vya kusambaza maji ilikuwa na changamoto nyingi”, walisema wakulima hao.

Katibu wa idara ya unyunyizaji maji nchini Ephantus Kimotho alisema hatua hii itapunguza gharama za uendeshaji miradi kwa asilimia 70.

“Kwa mwezi ilikuwa ikitumia dizeli ya zaidi ya shilingi milioni 10, mamlaka ya unyunyizaji nchini imeweza kuunganisha na umeme na sasa mradi huu utakuwa ukiokoa asilimia sabini ya pesa hizo”, aliweka wazi Kimotho.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wadau wa sekta ya uvuvi walalamikia unyakuzi wa ardhi

Published

on

By

Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uchumi wa bahari na masuala ya ubaharia imewataka wawekezaji wote waliovamia ardhi zilizotengewa

Kauli hii ilijiri baada ya wavuvi na wasimamizi wa fuo za bahari kuelekeza lalama zao kwa kamati hiyo wakidai kuhangaishwa kila mara na baadhi ya mabwenyenye wanaodaiwa kushirikiana na baadhi ya maafisa wa serikali.

Walidai kwamba unyakuzi huo umekuwa donda sugu na uliadhiri pakubwa shughuli za uvuvi huku wakiitaka serikali ya kitaifa kuingilia kati na kuhakikisha ardhi hizo zinarudhishwa mikononi mwa jamii za wavuvi haraka iwezekanavyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo na ambaye pia ni mbunge wa Marakwet Mashariki David Kangogo Bowen alisema ujenzi wa kibinafsi katika maeneo ya mita 60 kutoka ukingo wa bahari ni ukiukaji wa sheria kwani maeneo hayo yametengwa mahususi kwa matumizi ya wavuvi.

“Wale wamejenga mita 60 kando ya bahari waondolewa ndio hawa wavuvi wapewe nafasi ya kufanya biashara yao vizuri na pia wapate sehemu ya kuegeza maboti yao”. … alisisitiza David Bowen.

Kauli yake iliungwa mkono na mbunge wa Matunga Kassim Sawa Tandaza aliyesema agizo hilo ni sharti litekelezwa mara moja na yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Business

Maonyesho ya Kilimo Mombasa 2025 kuangazia uhifadhi wa mazingira

Published

on

By

Washirika kutoka mataifa saba duniani wanatarajiwa kushiriki katika maonyesho ya kimataifa ya kilimo ya mwaka 2025 yanayofanyika eneo la Mkomani kaunti ya Mombasa.

Mwenyekiti wa maonyesho hayo Henry Nyaga, alidokeza kuwa maonyesho hayo yamevutia washirika kutoka mataifa ya afrika mashariki, vile vile mataifa ya India, China, Botswana, Zambia na DR.Congo.

Akizungumza na Coco Fm katika uwanja wa maonyesho hayo, Nyaga alisema maonyesho ya mwaka huu wa 2025 yanaangazia kilimo biashara akisistiza umuhimu wa vijana kushiriki katika hafla hiyo iliyoambatanishwa na matumizi ya teknolojia na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhifadhi mzaingira.

“Kuna wale kutoka mataifa saba ambao tayari wameonyesha watakuwa nasi, tayari amewasili yule ambaye anatoka nchi ya Botswana, tunazingatia mambo haya ya tabia nchi ambayo yamefanya ulimwengu umekuwa tofauti sasa, kwa hivyo tunatarajia washiriki wote watatuonyesha jinsi gani tunaweza kukabiliana na hali hii ya mabadiliko ya tabia nchi, na ningependa haswa vijana muweze kufika hapa katika maonyesho kwa sababu kuna mengi ya kiteknolojia ambayo yanaweza kuwasaidia”,alisema Nyaga.

Kwa upande wake mwenyekiti wa maonyesho ya kilimo nchini Edith Onzare pamoja na mwanachama wa baraza la maonyesho ya Kilimo Mombasa- Anisa Abdhalla waliwasihi wananchi kutumia fursa hiyo kujifunza mengi kuhusu kilimo endelevu na namna ya kujiendeleza kuhusu ufugaji wa kisasa.

“Njooni kwa wingi tutajifunze mengi ya kilimo, kuna mifugo ya aina mbali mbali kuna kilimo na teknolojia hasa kwa vijana wetu, magen z kuna kazi nyingi ambazo ukija hapa kwenye maonyesho utajifunza mambo mengi ya kiteknolojia na taaluma mbali mbali ambazo utaweza kupata usaidizi”,walisema viongozi hao.

Baadhi ya washirika katika maonyesho hayo walishinikiza wakenya kukumbatia kilimo cha kisasa katika kuboresha mapato vile vile kulinda mazingira.

Wakiongozwa Benson Muchiri, waliwahimiza wakulima kujitenga na mbinu za jadi za kupalilia mashamba, akisema zimekuwa zikichangia mazao duni.

Muchiri ambaye amekuwa akitumia chupa na mabomba ya maji yaliyorushwa kuandaa sehemu za kuotesha mbegu kabla ya upanzi, amesema mbinu hiyo inasaidia kuokoa matumizi ya ardhi ipasavyo, sawa na kuhifadhi mazingira.

“Ninataka kuonyesha wakulima jinsi ya kufanya kilimo cha mjini, sio lazima uwe na kipande kikubwa cha ardhi ndio ufanye ukulima hasa kilimo cha mboga, ukiangalia vile vitu tulivyotumia hapa ni vile ambavyo ni kero, ukiangalia tuna chupa za plastiki ambazo tumezitumia, kile ambacho kinachafua mazingira hicho ndio tunahimiza mkulima badala ya hicho kitu kipotee wacha kiwe faida kwako”,alisema Muchiri.

Zaidi ya washirika 200 wanahudhuria maonyesho hayo ambayo yanaanza rasmi Jumatano 3 Septemba 2025, na kukamilika Jumapili 7 Septemba 2025.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending