Business
Wahudumu wa Tuktuk walalamikia kupanda kwa bei ya mafuta

Wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa Tuktuk katika wadi ya Mariakani eneo la bunge la Kaloleni kaunti ya Kilifi wanaendelea kulalamikia gharama ya juu ya bei ya mafuta ya petroli hali ambayo imeathiri biashara zao.
Kulingana na baadhi ya wahudumu hao, bidhaa zisizo na msingi zimeshuka bei ilhali bei ya mafuta ikionekana kuendelea kupanda jambo ambalo walisema imekuwa changamoyo wa wahubumu wengi.
Wakizungumza na Coco Fm , wahudumu hao wa Tuktuk walidai kwamba tangu kuongezwa kwa bei ya mafuta ya Petroli kwa shilingi nane wengi wao wamepata changamoto hata zaidi huku wakipoteza wateja baada ya kujaribu kuongeza nauli kwa wateja wao.
Hata hivyo, waliitaka serikali kuu kuingilia kati swala hilo mara moja kwani asilimia kubwa ya wahudumu hao wanaendelea kupata hasara.
Wakati huo huo walipendakaza bidhaa ambazo sio muhimu kama vile sigara na Pombe kuongezwa bei na na kupunguza bei za mafuta na vyakula.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Rais William Ruto aikabidhi bodi ya majani chai shilingi bilioni 2.65

Rais William Ruto ameikabidhi bodi ya majani chai shilingi bilioni 2.65 zilizopatikana kwa benki ambazo zimeshindwa kujiendeleza.
Pesa hizo zilitoka kwa benki ya Chase na Benki ya emperial ambazo zilikuwa zimechukua pesa za wakulima wa majani chai kote nchini.
Kupitia shirika la bima wakulima wa majani chai watalipwa fidia ya hasara iliyosababishwa na kuporomoka kwa benki hizo.
Akizungumza na zaidi ya wakulima 600,000 wa majani chai katika ikulu ya Nairobi rais Ruto alitaka bodi ya majani chai kuhakikisha kuwa pesa hizo zinawafikia wakulima.
Kama juhudi ya serikali kuimarisha sekta hiyo rais ruto alisema kuwa bei ya majani chai imeongezeka katika kipindi cha miaka miwili kutokana na mageuzi yaliyoletwa katika sekta hiyo.
Aidha alisema mapato ya majani chai yamepanda kutoka shilingi bilioni 138 mwaka wa 2022 hadi shilingi bilioni 215 mwaka 2024, huku serikali ikilenga kufikia shilingi bilioni 280 ifikapo mwaka 2027.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Bei ya vitunguu katika masoko ya humu nchini kuongezeka

Bei ya Vitunguu katika masoko ya humu nchini huenda ikaongezeka hata zaidi kufuatia uhaba wa bidhaa hiyo.
Kufuatia hatua hiyo wafanyibiashara wa vitunguu humu nchini wamelazimika kuagiza bidhaa hiyo kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.
Wakizungumza na vyombo vya habari, Wafanyibiashara hao walisema kuna uhaba mkubwa wa vitunguu jambo ambalo limefanya bei kupanda.
Kulingana na wakulima wa zao hilo, hawakupanda vitunguu kutakana na gharama ya juu ya mbegu pamoja na changamoto za mabadiliko ya hali ya anga.
Aidha walisema kuwa gharama ya Kilimo cha vitunguu imekuwa juu ikilinganishwa na mapato ya chini na ukosefu wa bei nzuri sokoni.
Taarifa ya Pauline Mwango
-
Entertainment8 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment20 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News17 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni