Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Matunda Malindi Walalamikia Kudorora kwa Biashara Kutokana na Ukosefu wa Soko

Published

on

Wafanyabiashara wa kuuza matunda karibu na soko la Kwa Jiwa mjini Malindi, Kaunti ya Kilifi, wanalalamikia kushuka kwa biashara yao kutokana na uhaba wa wateja katika eneo hilo.

Akizungumza na mwanahabari wetu, Mshauri Mkuu wa chama cha Matunda Sales Group, Nathaniel Menza Chengo, amesema kuwa matunda yao yanaendelea kuharibika kila siku kwa kukosa wanunuzi, hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa biashara zao.

“Kwa sasa matunda ni mengi lakini hakuna soko. Tunapata hasara kubwa kwa sababu matunda yanaharibika kabla hatujayauza,” amesema Chengo.

Chengo ameitaka serikali ya kitaifa pamoja na serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kwa kujenga kiwanda cha kusindika matunda ili kuwawezesha kuuza bidhaa zao kupitia viwandani. Anasema hatua hiyo itasaidia kupunguza hasara na kuinua maisha ya wafanyabiashara katika eneo hilo.

Amebainisha kuwa kwa sasa, zaidi ya tani 10 za matunda huharibika kila siku kutokana na ukosefu wa soko la uhakika.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Vijana Kaunti ya Tana River Waanzisha Biashara ya Sambusa za Samaki kuinua Uchumi

Published

on

Vijana katika Kaunti ya Tana River wameanzisha biashara ya upishi wa sambusa za samaki kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kwa kutumia rasilimali za baharini.

Wamebuni mbinu ya kipekee ya kuandaa sambusa kwa kutumia samaki wa aina mbalimbali, wakiwemo samaki papa. Mbali na sambusa, vijana hao pia wameweza kuunda bidhaa nyingine za thamani kutokana na samaki, hatua inayochochea ubunifu na kuongeza ajira miongoni mwao.

Kulingana na vijana hao, biashara hiyo inalenga kuongeza kipato chao na kufungua milango ya kuingia katika masoko mapya, ya ndani na hata ya nje ya kaunti.

Hatua hii imesukumwa na changamoto ya uhaba wa soko la samaki katika eneo hilo, hali ambayo husababisha uharibifu wa samaki kutokana na kukosa wanunuzi. Kwa hivyo, ubunifu huu umekuwa suluhisho la kiuchumi na kiteknolojia kwa vijana wa Tana River.

Continue Reading

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Matano Mane Waililia Serikali ya Kaunti ya Kilifi Kuwajengea Choo

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuwajengea choo, wakisema ukosefu wa huduma hiyo muhimu umekuwa kero kubwa inayozorotesha shughuli za biashara.

Wakiongozwa na Phelisia Mageshi, wafanyabiashara hao wamesema kuwa hali ya sasa imesababisha baadhi yao kuhamishia biashara zao nje ya soko hilo, kutokana na mazingira yasiyofaa kwa shughuli za kila siku.

Bi Mageshi ameeleza kuwa licha ya serikali ya kaunti kufahamishwa kuhusu changamoto hiyo mara kadhaa, hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa hadi sasa, hali inayowafanya kuhisi kusahaulika.

Wameitaka serikali ya kaunti kuingilia kati kwa haraka ili kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kuhakikisha afya ya wananchi inalindwa.

Continue Reading

Trending