Business
Wadau wa Sekta ya Uchumi wa Baharini Waisihi Serikali Kuongeza Uwekezaji Pwani

Wadau katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa katika eneo la Pwani wameitaka serikali kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kusaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana wa eneo hilo.
Kwa mujibu wa wadau hao, serikali haijatoa kipaumbele cha kutosha kwa sekta hiyo, licha ya kuwepo kwa raslimali nyingi za bahari ambazo bado hazijatumika ipasavyo. Wamesisitiza kuwa uwekezaji wa kimkakati unaweza kufungua fursa nyingi kwa vijana, na hivyo kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira katika ukanda wa Pwani.
Viongozi hao pia wameitaka serikali, kupitia wizara husika, kuweka mikakati ya wazi na ya utekelezaji ili kuhakikisha kwamba wananchi—hasa vijana—wanapata nafasi ya kunufaika na uchumi wa buluu.
Wakati huo huo, wamewahimiza vijana wa Pwani kujipanga na kujitolea kwa dhati, ili wawe tayari kutumia fursa zinazojitokeza katika sekta ya uchumi wa bahari kwa manufaa yao binafsi na ya jamii kwa ujumla.
Sekta ya uchumi wa buluu inazidi kutambuliwa kama eneo muhimu la ukuaji wa uchumi, hasa kwa maeneo ya pwani yanayozungukwa na bahari, mito na maziwa makuu.
Business
Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.
Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.
Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.
Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.
Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .
Business
Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.
Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.
Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.
Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.