Connect with us

Business

Viongozi wa Mombasa Waisihi Serikali Kuu Kuwekeza Zaidi Katika Uchumi wa Samawati

Published

on

Viongozi wa kaunti ya Mombasa wameitaka serikali kuu kuongeza uwekezaji katika sekta ya uchumi wa raslimali za baharini na maziwa, ili kuinua maisha ya wakazi wa Pwani na kuchangia katika kukuza pato la taifa.

Wakiongozwa na Seneta maalum Miraj Abdillah, viongozi hao wameeleza kuwa ipo haja ya haraka ya kuanzishwa kwa chuo cha mafunzo ya ubaharia katika eneo la Pwani, hatua itakayowawezesha vijana kupata ujuzi muhimu na fursa za ajira katika sekta ya baharini.

Akizungumza na wanahabari, Seneta Miraj alisema kuwa licha ya Pwani kuwa na raslimali nyingi za bahari, vijana wengi bado wanakabiliwa na ukosefu wa ajira na kutokuwa na nafasi ya kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi ya eneo hilo.

Viongozi hao pia wameitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuhakikisha kuwa wavuvi wanapatiwa vifaa vya kisasa, ili kuongeza ufanisi na tija katika shughuli zao za kila siku za uvuvi.

Kwa pamoja, walisisitiza kuwa sekta ya uchumi wa buluu ina uwezo mkubwa wa kubadilisha maisha ya watu wa Pwani, iwapo itawekewa vipaumbele vya kimkakati na uwekezaji wa kutosha kutoka kwa serikali zote mbili—kaunti na taifa.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Vijana Kaunti ya Tana River Waanzisha Biashara ya Sambusa za Samaki kuinua Uchumi

Published

on

Vijana katika Kaunti ya Tana River wameanzisha biashara ya upishi wa sambusa za samaki kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kwa kutumia rasilimali za baharini.

Wamebuni mbinu ya kipekee ya kuandaa sambusa kwa kutumia samaki wa aina mbalimbali, wakiwemo samaki papa. Mbali na sambusa, vijana hao pia wameweza kuunda bidhaa nyingine za thamani kutokana na samaki, hatua inayochochea ubunifu na kuongeza ajira miongoni mwao.

Kulingana na vijana hao, biashara hiyo inalenga kuongeza kipato chao na kufungua milango ya kuingia katika masoko mapya, ya ndani na hata ya nje ya kaunti.

Hatua hii imesukumwa na changamoto ya uhaba wa soko la samaki katika eneo hilo, hali ambayo husababisha uharibifu wa samaki kutokana na kukosa wanunuzi. Kwa hivyo, ubunifu huu umekuwa suluhisho la kiuchumi na kiteknolojia kwa vijana wa Tana River.

Continue Reading

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Matano Mane Waililia Serikali ya Kaunti ya Kilifi Kuwajengea Choo

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuwajengea choo, wakisema ukosefu wa huduma hiyo muhimu umekuwa kero kubwa inayozorotesha shughuli za biashara.

Wakiongozwa na Phelisia Mageshi, wafanyabiashara hao wamesema kuwa hali ya sasa imesababisha baadhi yao kuhamishia biashara zao nje ya soko hilo, kutokana na mazingira yasiyofaa kwa shughuli za kila siku.

Bi Mageshi ameeleza kuwa licha ya serikali ya kaunti kufahamishwa kuhusu changamoto hiyo mara kadhaa, hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa hadi sasa, hali inayowafanya kuhisi kusahaulika.

Wameitaka serikali ya kaunti kuingilia kati kwa haraka ili kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kuhakikisha afya ya wananchi inalindwa.

Continue Reading

Trending