International News
Tume ya uchaguzi ya Tanzania INEC yazima ndoto ya Luhaga Mpina

Tume huru ya uchaguzi nchini Tanzania (INEC) imekiandikia chama cha upinzani cha ACT Wazalendo kuwa hakitaweza kumteua mgombea wa urais kupitia chama hicho, Luhaga Mpina.
Katika barua ambayo INEC imeiandikia ACT-Wazalendo, tume hiyo ya uchaguzi ilirejea uamuzi wa Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa uliotolewa siku ya Jumatano Agosti 27, 2025 ambao ulisema mgombea wa urais wa chama hicho Luhaga Mpina, hakukidhi matakwa ya Katiba na kanuni za ACT kuwania nafasi hiyo.
ACT-Wazalendo walipokea barau kutoka kwa msajili wa vyama vya kisiasa kujieleza jinsi ilivyoendesha mchakato wa kumpata mgombea wake wa urais kama yalivyokuwa madai ya mwanachama wa chama hicho, Manalisa Ndala.
Barua hiyo ya INEC ilihitimisha kwa kueleza kwamba inafuta barua yake ya Agosti 15,2025 kuhusu urejeshaji wa fomu kwa mgombea na kumtaka asifike katika ofisi hizo kwa ajili ya uteuzi.
Hata hivyo, chama cha ACT-Wazalendo kilisema kwenye taarifa yake kwamba kinaupinga uamuzi wa Ofisi ya majili na pia kilisema Tume ya uchaguzi ilijiongoza vibaya kwenye kukubaliana na kile uchaguzi mkuu Tanzania kufanyika Oktoba 29.
Chama cha ACT- Wazalenzo kilishikilia kwamba maagizo ya msajili mkuu wa vyama vya kisiasa ni kinyume na matakwa ya kikatiba yanayoitangaza Tume hiyo kuwa ni huru na isiyochukuwa amri kutoka chombo chochote kile.
Katika taarifa hiyo, Katibu mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu, aliiomba Tume ya Uchaguzi kubadilisha uamuzi wake na kutokuifanya ionekane kutokuwa huru kwenye utekelezaji wa kazi zake kisheria.
Hata hivyo mgombea wa urais wa chama cha CCM, Samia Suluhu Hassan na chama cha upinzani cha NRA, Hassan Kisabya Almas, walikamilisha hatua ya uteuzi na kukabidhiwa magari aina ya Landcruiser ambayo watayatumia katika kampeni zao za uchaguzi zinazotarajia kuzinduliwa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
International News
Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.
Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.
Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.
Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.
Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Kampeni za uchaguzi mkuu za shika kasi Tanzania

Mgombea wa wadhfa wa Rais wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama cha Mapinzudi CCM taifa Dkt Samia Suluhu Hasssan anaendeleza kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho.
Rais Samia Suluhu, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kutoka chama tawala CCM, wamo katika harakati za kuwashawishi wapiga kura ili kuwachagua kuliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine ya miaka mitano ijayo.
Siku ya Alhamis tarehe 11 Septemba 2025, Rais Samia Suluhu alifanya mkutano mkubwa wa siasa katika eneo la Urambo mkoani Tabora, ambako alizungumzia zaidi ufanisi wa maendeleo akisema umetokana na utawala bora wa chama cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa hayo ni kuboreshwa kwa muundo misingi ya barabara, afya na ustawi wa uchumi na biashara, na kutaja kimakusudi zao la Tumbaku linalokuzwa kwa wingi mkoani Tabora.
Rais Samia alisema kuwa kunaongezeko kubwa la pato linalotokana na zao la Tumbaku ambapo sasa linauzwa kwa dola 2.5 kutoka bei ya zamani ya dola 1 kwa tani moja.

Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania katika mji wa Urambo mkoa wa Tabora {picha kwa hisani}
Kwa upande wake, Mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi alikuwa katika mkoa wa Katavi, kusasambua yale serikali ya Mama Samia Suluhu imepanga kuyatimiza punde tu itakapochaguliwa kuwaongoza Watanzania.
Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025.
Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.
Taarifa ya Eric Ponda