Connect with us

News

Tume ya huduma za polisi (NPSC) kuajiri maafisa wa polisi 10,000

Published

on

Tume ya kitaifa ya huduma za polisi (NPSC) imehakikishia wakenya kwamba zoezi lijalo la kuwaajiri maafisa wa polisi litakuwa wazi, shirikishi, na lisilo na utovu wa nidhamu.

Akiwa mbele ya kamati ya usalama ya bunge la kitaifa hapo jana Jumanne, afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo Peter Leley alisema hatua zimewekwa ili kuhakikisha haki, ikiwa ni pamoja na matumizi ya waangalizi huru na zana za kidijitali.

Leley aliongeza kuwa uajiri huo pia utalenga jamii zilizo na uwakilishi mdogo na zilizotengwa kulingana na sera za kuchukua hatua.

Alisema tume hiyo imeshirikisha wadau wakuu, akiwemo katibu wa baraza la mawaziri wa mambo ya ndani, ambaye mchango wake umeingizwa katika mfumo wa ugawaji wa zoezi hilo.

NPSC inalenga kuajiri maafisa wa polisi 10,000 chini ya kanuni mpya iliyoundwa ili kukuza uwazi baada ya mazoezi ya hapo awali kugubikwa na malalamiko ya hongo na upendeleo.

Kati ya nafasi 10,000, nafasi 4,000 zimehifadhiwa kwa ajili ya vijana waliohitimu kutoka huduma ya kitaifa ya vijana (NYS).

Kwa mara ya kwanza, zoezi hilo litafanyika kupitia njia ya mtandao.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Macharia: Jamii ya Kilifi kusini watapeliwa ardhi kufuatia ukosefu wa Elimu

Published

on

By

Msaidizi wa Kamishna wa kaunti ya Kilifi eneo la Kilifi Kusini, Francis Macharia amesema ukosefu wa elimu umechangia kwa wanajamii wengi kaunti ya Kilifi kutapeliwa katika umiliki wa ardhi.

Akizungumza eneo la Vipingo, Macharia alisema kuwa wanajamii wengi hasa wazee wamekuwa wakitapeliwa mashamba yao kutokana na kukosa kisomo.

Macharia alisisitiza haja ya jamii kuzingatia elimu kwani visa vya ulaghai wa mashamba kutokana na ukosefu wa elimu vimekithiri mno hasa mashanani.

“Kuna baadhi ya vijana pia wamekuwa wakiwatapeli wazazi wao fedha za inua jamii pindi zinapotumwa, na hii imechangiwa na kutosoma wazee hao” aliongeza Macharia.

Macharia alisema wazazi pia wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa wanao wanapata elimu ipasavyo akisema kuwa eneo la Kilifi kusini limekuwa na visa vingi vya watoto wanaoacha shule na kuingilia vibarua.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Makalo atoa wito kwa serikali kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Kasighau kaunti ya Taita Taveta Amos Makalo ametoa wito kwa serikali kuu kuendeleza mpango wa ugavi wa chakula cha msaada katika eneo hilo sawa na maeneo mengine kote nchini ili kunusuru maelfu ya wananchi wanaokabiliwa na baa la nja.

Makalo alisema chakula hicho ni kidogo mno kwani wananchi wengi wa Kasighau pamoja na maeneo mengine ya kaunti hiyo wanakabiliwa na baa la njaa.

Wakati huohuo Makalo alimshinikiza mwakilishi wa kike kwenye kaunti hiyo Lydia Haika kuishawishi serikali kuu kuikumbuka kaunti hiyo katika kupeana misaada mbalimbali ambayo itawafaidi wenyeji.

“Wananchi wanahangaika kutokana na njaa. Na kwasababu umetutembelea na mazuri leo wacha niombe kwamba hayo Mazuri yaendelee kwa muda huu ulio mbele yetu maana hali ni ngumu sana’’

Haya yanajiri huku Serikali ya kitaifa kupitia wizara ya huduma za kitaifa na mipango maalum ikiendeleza shughuli za usambazaji wa chakula cha msaada kwa wahanga wa baa la njaa kaunti ya Taita Taveta na maeneo mengine nchini.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending