Connect with us

Sports

Tukitolewa Makundi Tutakua Tumefeli Kocha Jaribuni Sec

Published

on

Mkufunzi wa Shule Ya Upili ya Jaribuni Hassan Pande amesema kwmaba iwapo watabanduliwa kwenye hatua ya makundi mashindano ya Shule za Upili ukanda wa Pwani Mpeketoni Lamu Julai 2.

Akizungumza ndaani ya Kipenga Cha Coco FM mwalimu huyo amekiri kutokana na malengo ambayo wameweka msimu huu kutoka kwenye awamu ya makundi au hata nusu fainali kama shule watakua wamefeli kwani lengo lao ni kuwakilisha ukanda huu Kitaifa mwaka huu.

“Sisi si ati kutolewa Makundi ata tukitolewa Semis tutakua tumefeli mno,tumeweka investment kubwa katika timu yetu na mwalimu mkuu amewaweka vijana sawa sawa letu ni kupata matokeo mazuri na kufuzu kitaifa.”

Kuhusu mchezo wao kuelekea mashindano hayo katika kaunti ya Lamu mwalimu huyo ameongezea kuwa mashabiki watarajie Jaribuni Tofauti na ilivyokua katika mashindano ya Kaunti.

“Mechi za Regionals najua si kama za kaunti High Intensity,kasi nyingi na mpira mwingi kwa hivyo mashabiki watarajie Jaribuni mpya kabisaa kuelekea Lamu.”

Jaribuni wamejumuisha Kundi B pamoja na : Mokowe,Serani na Tana.

Mashindano hayo yanaanza Julai 2 hadi Jula 4 Mpeketoni Lamu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending