Entertainment
Simon Kabu na Sarah ‘Mtalii’ Wazua Gumzo Mpya: Mapenzi Yamerudi Moto Tena?

Kwa mara nyingine tena, majina ya Simon Kabu na Sarah ‘Mtalii’ Njoki yamerudi kwenye vichwa vya habari, baada ya video ya hivi karibuni kusambaa mtandaoni na kuwasha moto wa tetesi mpya.
Simon, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bonfire Adventures, alichapisha video kwenye Facebook yake, ikimuonesha akiwa katika matembezi ya kifahari ndani ya yacht jijini Dar es Salaam. Lakini kilichovutia zaidi si yatch wala anga ya usiku ya Dar—bali ni uwepo wa Sarah, mkewe wa zamani ambaye walitangaza kuachana miezi kadhaa iliyopita.
Wakiwa pamoja na wanandoa wengine, Simon na Sarah walionekana wakifurahia muda wao kama hakuna jambo lililotokea hapo awali. Wakiwa wamevalia mavazi ya likizo, walionekana wakicheza pamoja densi ya ‘Wa Wa Wa in the World’—densi iliyoenea kutoka Uganda—huku tabasamu likiwa limewavaa wote wawili. Gauni la neti jeupe alilovaa Sarah lilionekana kumng’ara kwa mvuto, huku Simon akijichanganya kwa kaptura na T-shirt yake ya kawaida.
Katika kipande kingine, Simon anaonekana akiburudika kwa densi pamoja na rafiki yake, akiwasisimua wanawake waliokuwa wameketi karibu. Huu haukuwa usiku wa kawaida—ulikuwa ni usiku wa kusherehekea ushindi mkubwa wa Bonfire Adventures, baada ya kutangazwa kuwa Shirika Bora la Usafiri na Utalii nchini Kenya kwa mwaka 2025 na World Travel Awards.
Simon aliandika kwa ucheshi: “Sherehe za Bonfire Adventures kushinda tuzo ya Kenyans Leading Tours and Travel Agency 2025 ziliendelea hadi usiku wa Jumapili ndani ya yacht huko Dar es Salaam. Nani alicheza vizuri zaidi?”
Wafuasi wake mtandaoni hawakubaki kimya. Wengi walijawa na furaha, wengine wakiwa na maswali: Je, ni dalili ya mapenzi kuhuishwa? Au ni urafiki tu wa zamani uliorejea kwa ustaarabu?
Mojawapo ya maoni maarufu kwenye video hiyo liliandika: “Hii siyo tu densi, hii ni lugha ya mapenzi isiyohitaji maneno.”
Kwa sasa, hakuna tamko rasmi kutoka kwa wawili hao kuhusu hali ya uhusiano wao. Lakini jambo moja ni wazi—video hii imefungua ukurasa mpya wa mjadala kuhusu maisha ya wawili hawa ambao kwa muda mrefu wamekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii.
Entertainment
Sijakataa Kuchangiwa, Ila Nipewe Heshima, Nyevu Fondo Afunguka

Muunda maudhui maarufu Pwani, Nyevu Fondo, amefunguka sababu zake za kukataa pesa za mchango wa matibabu zilizochangishwa na Presenter Jakki.
Presenter Jakki, bila kumjulisha Nyevu, alianzisha kampeni ya mchango wa matibabu kwa jina lake baada ya kujua Nyevu anaugua, akiwahamasisha mashabiki na wafuasi wake kutuma msaada wa fedha akishiriki picha za Nyevu Fondo kwenye mitandao ya kijamii.
Akizungumza hewani kwenye kipindi cha Janjaruka 254, Nyevu alisema wazi kuwa hana tatizo na watu kumchangia, lakini alikerwa na jinsi jambo hilo lilivyofanywa bila ushauriano:
“Mimi sijakataa kuchangiwa. Ni kitu poa. Kitu ambacho kinaniumiza ni kuwa kwa nini hakuniuliza mimi mwenyewe, naugua nini na nahitaji msaada aina gani? Je, ule ugonjwa unahitaji msaada wa aina gani ama kile kitu nachougua kinahitaji msaada ama ala?”
Awali kwenye ukurasa wake wa Facebook Nyevu Fondo aliandika;
Hata hivyo Presenter Jakki hajanyamaza. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Jakki amejibu kwa hisia nzito, akieleza kusikitishwa na jinsi nia yake njema ilivyotafsiriwa vibaya mbele ya umma.
Hapa chini ni kauli yake kamili:
“Binadamu mbona tuna roho nyepesi kama korosho? 😢 Kwa nini mnanitengenezea taswira mbaya mbele ya hadhira yangu, ilhali nia yangu ilikuwa njema? Sitaki sifa wala umaarufu—nilitaka kusaidia kwa moyo wa huruma. Kumbukeni, kuna leo na kesho… na mitandao haitasahau kamwe. INTERNET NEVER FORGETS.”
“Kwa kuwa Nyevu Fondo hajaweza kupokea mchango huu, nimeamua pesa hizi nizielekeze kwenye kituo cha watoto yatima (Children’s Home) zikawe baraka kwa wengine. Labda Mungu ataniona na kunibariki. Kwa yote, nawaombea baraka – watu wa Mungu tuchukuliane kwa upendo.”
Awali Nyevu aliandika
Entertainment
Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.
Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”
Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.
Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.
Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.
Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.