Entertainment
Sean “Diddy” Combs Atahukumiwa Katika Kesi Itakayosikilizwa Oktoba 3

Wiki iliyopita, Combs alipatikana na hatia kwa makosa mawili ya usafirishaji kwenda kufanya ukahaba baada ya kesi ya wiki nane. Anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka kumi jela kwa kila kesi, ingawa wachambuzi wa sheria wanatabiri kuwa atapata kidogo zaidi.
Aliondolewa mashtaka mazito zaidi ambayo alishutumiwa kula njama ya ulaghai na biashara ya ngono.
Baada ya uamuzi huo kutangazwa Jumatano iliyopita ya tarehe 2/7/2025, Jaji Arun Subramanian alipendekeza kuratibiwa kusikilizwa kwa hukumu hiyo Oktoba 3, lakini aliambiwa na mawakili wa Combs kwamba wanatarajia kuharakisha mchakato huo wa hukumu.
Awali mawakili wa Combs walipendekeza tarehe 22 Septemba kwa ajili ya kusikilizwa kwa hukumu, lakini baadaye walirekebisha pendekezo lao hadi Oktoba 3 katika barua iliyofuata kwa hakimu muda mfupi baadaye.
Barua ya kwanza ilisema pendekezo la utetezi lilikuwa chini ya idhini kutoka kwa ofisi ya uangalizi. Barua ya pili, ambayo kimsingi iliunga mkono msukumo wao wa kuharakisha hukumu yake, ilirejesha kikao cha hukumu hadi tarehe yake ya awali na kusema ofisi ya uangalizi haikupinga ratiba hiyo.
Mawakili na Combs walipiga simu iliyodumu chini ya dakika moja baada ya naibu wa Subramanian kuwaambia mawakili kwamba hakimu atawajibu kuhusu tarehe yao iliyopendekezwa.
Waendesha mashtaka walikuwa walimshtaki Combs kwa kuongoza biashara ya uhalifu ambapo alidaiwa kutumia vitisho, vurugu, kazi ya kulazimisha, hongo na uhalifu mwingine kuwashurutisha rafiki zake wa kike wa zamani Cassie Ventura na mwanamke ambaye alitoa ushahidi kwa jina bandia la Jane kujihusisha na maonyesho ya ngono yaliyochochewa na wasindikizaji wa kiume wanaoitwa “Freak Offs”
Combs alikana mashtaka hayo huku mawakili wake walidai kuwa kile kinachojulikana kama “Freak Offs” kilikubaliwa kutokana na uhusiano wake wa muda mrefu na Ventura na Jane.
Combs pia anakabiliwa na mashtaka kadhaa ya kiraia, ambayo alikanusha makosa yote.
Mkali huyo wa muziki amekuwa kizuizini katika gereza la shirikisho la Metropolitan Detention Center huko Brooklyn tangu alipokamatwa mwezi Septemba 2024.
Taarifa na Francos Mzungu
Entertainment
Mboga Imejileta; Arrow Bwoy Aitisha Pigano Dhidi ya Shakib

Msanii maarufu wa Kenya, Arrow Bwoy, amezua gumzo mtandaoni baada ya kumualika wazi wazi mfanyabiashara kutoka Uganda, Shakib Cham, kwenye pambano la ndondi.
Hii imekuja baada ya kipigo cha hadharani ambacho Shakib alipokea kutoka kwa msanii mwenzake wa Uganda, Rickman, hali iliyoacha mashabiki wengi wakisema: “Sasa ata Arrow Bwoy anaweza!”
Kupitia video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Arrow Bwoy, anayefahamika kwa vibao kama Digi Digi, hakuonyesha woga wowote. Kwa ucheshi, alisema amekuwa akisubiri nafasi kama hii kwa muda mrefu.
“Mboga imejileta,” alisema kwa kujiamini, akimaanisha kuwa Shakib amejileta mwenyewe kwenye kipigo.
“Chakula kiko tayari. Niko tayari kwa pambano hili.”
Arrow Bwoy pia hakusita kumtaja mke wa Shakib, Zari Hassan, akimtaka akae mbali na ulingo siku ya pambano hilo kwa usalama wake binafsi.
“Zari, usijisumbue kuja. Hii si sehemu ya wanawake. Usije ukazimia tukapata janga la pili,” alisema kwa kejeli.
Hata hivyo, wakosoaji wake walikumbusha jamii kuhusu video za awali zinazoonyesha Arrow Bwoy akichapwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Swali likabaki: Je, kweli ana uwezo wa kumpiga Shakib au ni porojo za mitandaoni?
Kwa jina la Zari kuingizwa kwenye sakata hili, mvutano umeongezeka na mashabiki kote Afrika Mashariki wanasubiri kuona kama Shakib atakubali changamoto hii ya kihistoria.
“Zari, kama unasikia, mtume tu kijana wako aje achukue kichapo — kichapo cha kimataifa,” Arrow Bwoy alimalizia kwa msisitizo.
Kwa sasa, macho yote yako kwa Shakib. Je, atakubali changamoto hii na kuweka historia mpya ya burudani Afrika Mashariki?
Entertainment
#CHAN2024: Savara, Zuchu na Eddy Kenzo Kutumbuiza Fainali ya CHAN 2024 Nairobi

Mashindano ya CHAN 2024 yakielekea ukingoni, mashabiki wanatarajiwa kupata burudani ya aina yake kutoka kwa baadhi ya nyota wakubwa wa muziki Afrika Mashariki.
Kenya, Uganda na Tanzania zitawakilishwa vilivyo kupitia majina makubwa matatu: Savara wa Kenya (mwanachama wa zamani wa kundi maarufu Sauti Sol), Eddy Kenzo wa Uganda, na Zuchu kutoka Tanzania, anayejulikana kwa jina halisi Zuhura Othman.
Onyesho hili la kufunga pazia litafanyika sambamba na mechi ya fainali Jumamosi, likitarajiwa kuhamasisha na kuburudisha maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanja wa Kasarani. Shoo hiyo inalenga kumaliza mashindano haya ya kihistoria kwa upekee na kiwango cha juu cha burudani.
Mbali na kusubiriwa kwa hamu jukwaani, Savara pia amekuwa na mchango mkubwa nyuma ya pazia. Yeye ndiye mtunzi na mtayarishaji wa wimbo rasmi wa CHAN 2024 unaoitwa “Pamoja”.
Wimbo huo unashirikisha nyota kutoka kanda hii: Elijah Kitaka wa Uganda na Phina wa Tanzania. Uliimbwa kwa mara ya kwanza katika sherehe za ufunguzi na uliweka ladha na hamasa ya mashindano haya.
Ingawa wenyeji wa mashindano haya—Kenya, Uganda na Tanzania—waliishia katika hatua ya robo fainali, fainali za mwaka huu zinaahidi kuwa kilele cha msisimko.
Burudani kutoka kwa Zuchu, Savara na Eddy Kenzo itakuwa chachu ya kuhitimisha mashindano yaliyojaa matukio na hisia.
Kwa upande mwingine, kumekuwa na malumbano mitandaoni kati ya mashabiki wa Kenya na Tanzania, hususan baada ya timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, kudondoshwa nje ya michuano hiyo katika robo fainali.
Mashabiki wa Tanzania hawakusita kuchokoza wenzao kwa kejeli, jambo lililoongeza ladha ya ushindani wa nje ya uwanja.