News
Rais Ruto Awaomba Radhi Watanzania.

Rais William Ruto amejitokeza na kuomba msamaha kwa niaba ya vijana wa Gen Z dhidi ya utawala wa Serikali ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Rais Ruto ameisihi serikali ya Tanzania kuondoa hofu kuhusu Mabishano makali ya Mtandaoni baina ya mataifa haya mawili licha ya Viongozi wa mataifa haya mawili Rais William Ruto na Mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuonekana kujaribu kuuzima moto wa mashambulio ya mitandaoni hasa miongoni mwa vijana wa Gen Z.
Akizungumza wakati wa dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa yaliondaliwa jijini Nairobi, Rais Ruto amesema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano mwema wa kidiplomasia na wala sio kuchangia uhasama, akiwaomba msamaha pia vijana wakenya.
Viongozi wahudhuria dhifa ya asubuhi ya maombi ya kitaifa
Kauli ya Rais Ruto imejiri baada Bunge la Tanzania kulazimika kusitisha vikao vya kawaida na kujadili hoja inayotajwa kugusia usalama wa taifa la Tanzania huku wakimpongeza rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua aliyochukua ya kuwafurusha Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wakiongozwa na Martha Karua ambaye kiongozi wa chama cha People’s Liberation Party nchini Kenya na Jaji Mkuu mstaafu Willy Mutunga, Mwanaharakati Boniface Mwangi wa Kenya na Agather Atuhaire wa Uganda.
Mwanaharakati Bonifance Mwangi alipatikana katika eneo la mpakani mwaka Kenya na Tanzania katika eneo la Lunga lunga ilihali mwenzake Agather Atuhaire akipatikana karibu na kituo cha mpakani na Mtukula.
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi