Connect with us

Sports

Msururu Wa Raga Driftwood 7s Umengoa Nanga Mombasa

Published

on

Mashindano ya kitaifa ya misururu ya Raga nchini mwaka 2025 yameongoa nanga mjini Mombasa, Msururu huo wa kwanza wa Driftwood 7s inafanyika katika uwanja wa Mombasa Sports Club.

Jumla ya timu 26 zinashiriki katika makundi ya wavulana na wasichana wa chini ya umri wa miaka 18 na 15, na kundi la pamoja kwa walio chini ya miaka 13, yakionyesha kizazi kipya cha vipaji vya raga nchini Kenya.

Katika mashindano ya Divisheni ya Kwanza, mabingwa watetezi Kenya Harlequins wako Kundi A dhidi ya MMUST, KU Blak Blad, na Mwamba RFC,

Kundi B linajumuisha Kabras Sugar RFC,Catholic Monks, Nakuru RFC, na Impala RFC, kundi C linajumuisha KCB RFC, Nondescripts RFC, Daystar Falcons, na wenyeji MSC Rugby huku Kundi D litakuwa na ushindani mkali kati ya Menengai Oilers, Strathmore Leos, Stallions Rugby, na Kabarak University.

Kwa upande wa Division Two, timu 36 zinashiriki katika mashindano hayo, ambapo vigezo maalum vilitumika kugawa nafasi kwa vilabu wanachama wa KRU, timu kutoka ukanda wa pwani, zile zilizofanya vizuri awali, na zile zenye historia nzuri katika mashindano.

Makundi ya Division Two ni pamoja na AP Warriors, Kilifi Titans, Likoni, na Mean Machine ambao watacheza katika Kundi A; Embu RFC, Kaya Rugby, North Coast Stormers, na MKU Thika katika Kundi B; Homeboyz RFC, Jackals, NYS Eagles, na Makueni RFC katika Kundi C; Kisumu RFC, KCNP, NYS Spades, na Sigalagala NP katika Kundi D; huku South Coast Pirates, Vihiga Granites, Zetech Oaks, na Northern Suburbs wakicheza katika Kundi E.

Mechi ya fainali ya mashindano hayo itachezwa siku ya Jumapili mwaka huu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Kocha Wa Bafana Bafana Ataja Kikosi Cha Mwisho Cha CHAN

Published

on

By

AFRIKA KUSINI (SOUTH AFRICA)

Wanajiita Bafana Bafana kwa jina la Utani.
Afrika Kusini inaorodheshwa ya 56 msimamo wa kila mwezi wa shirikisho la soka ulimwenguni FIFA
Taifa hilo halijawahi kushinda taji la CHAN licha ya kushiriki mara tatu miaka ya  (2011, 2014, 2025)

Kocha mkuu wa taifa hilo anaitwa Hugo Broos Hata hivyo katika majukumu ya CHAN amepewa kocha Molefi Ntseki ambaye ni mchezaji wa zamani wa taifa hilo na pia amewahi kuvinoa vikosi vya wachezaji wachanga timu ya taifa pamoja na vilabu vya Kaizer Chiefs na Bloemfontein.
Kocha huyo ametaja wachezaji 14 ambao hawana vilabu katika kikosi alichokitaja cha wachezaji 25
Badhi ya wachezaji nyota ni pamoja na Neo Maema anayepiga na Mamelodi Sundowns.
Bafana Bafana wako kundi C pamoja na Algeria,Guinea,Niger na Uganda.
Continue Reading

Sports

Mwanamieleka Hulk Morgan Aaga Dunia Akiwa Na Umri Wa Miaka 71

Published

on

By

Mwanamieleka maarufu nchini Marekani Hulk Hogan amefariki hapo jana akiwa na umri wa miaka 71, Madaktari walithibitisha kifo chake hapo jana  huku chanzo cha kifo chake kikitajwa kuwa ni tatizo la moyo.

Majina yake kamili ni Terry Bollea akiwa ni mwanamieleka aliyetamba sana miaka za 80 na 90 kule Marekani.

Hogan aliumwa moyo akiwa nyumbani kwake Florida kisha kupelekwa Hospitali ambapo alipatwa na umauti.
Hata hivyo, Wiki chache tu zilizopita, mke wa Hogan, Sky, alikanusha uvumi wa kwamba Hogan alikuwa katika coma, akisema moyo wake ulipata nguvu na alikuwa na nafuu baada ya kutoka kwenye upasuaji.
Continue Reading

Trending