International News
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni

Mahakama kuu nchini Tanzania imemrejesha kwenye debe mgombea urais wa chama cha upinzani ACT wazalendo, Luhaga Mpina na kupindua maamuzi yaliyotolewa na tume ya uchaguzi nchini humo INEC.
Hii inamaana tume ya INEC ni lazima imjumuishe Mpina katika orodha ya majina ya watakaopigiwa kura, hatua itakayosababisha upinzani kwenye uchaguzi huo mkuu.
Hatua hii sasa inampa Mpina fursa ya kuanzisha kampeni za kutaka kumbandua mamlakani rais Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Octoba 29 mwaka 2025.
Kampeni za uchaguzi tayari zinaendelea nchini humo.
INEC ilimzuia mpina kugombe wadhifa wa urais mwezi Agosti 26, 2025 ikidai chama cha ACT Wazalendo kilikiuka taratibu za chama kwa kumsimamisha Mpina kuwania wadhifa huo.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwa katika kampeni za uchaguzi mkuu.
Katika uamuzi uliotolewa Alhamisi mwezi Septemba 11, 2025, jopo la majaji watatu mjini Dodoma liliagiza INEC kumuidhinisha Mpina kama mgombea wa urais.
Anatarajiwa kujumuika na wagombea wengine 16 kutoka vyama vidogo vya kisiasa katika mapambano hayo ya kuwania urais, ambao wote wanania ya kung’atua rais wa sasa Samia Suluhu Hassan mamlakani.
Chama cha Chadema kilizuiwa kugombea katika uchaguzi huo baada ya kiongozi wake Tundu Lissu kufunguliwa mashtaka ya uhaini.
Kiongozi wa upinzani wa Chadema Tundu Lissu akiwa mahakamani.
Rais Samia Suluhu Hassan alichukua hatamu za uongozi kama rais baada ya kifo cha John Pombe Magufuli mwaka 2021.
Taarifa ya Joseph Jira.
International News
Ghasia zatanda nchini Nepal licha ya marufuku ya kutotoka nje.

Marufuku ya kutotoka nje inaendelea kukiukwa nchini Nepal ambako ghasia za uharibifu wa mali na umwagikaji wa damu zinaendelea.
Serikali ya Waziri mkuu KP Sharma Oli, ilipinduliwa ndani ya masaa 48 baada ya kuzuka kwa maandamano hayo, ambapo waandamanaji waliokuwa na ghadhabu walivamia na kuteketeza makaazi ya Waziri mkuu Oli, pamoja na bunge la nchi hiyo.
Licha ya jeshi la nchi hiyo kutanganza hali ya tahadhari na marufuku ya kutotoka nje, Waandamanaji hao waliendelea kukiuka marufuku hiyo na kumiminika katika barabara za mji mkuu wa Kathmandu, huku wakiwashambulia maafisa wa usalama, lakini pia kulenga makaazi ya maafisa wakuu wa serikali, wakiwemo Wabunge na mawaziri huku wakiteketeza majumba na magari yao.
Kulingana na taarifa za maafisa wa usalama nchini humo, waandamanaji hao pia walivamia magereza na kuwaachilia huru jumla ya wafungwa elfu 13 katika kipindi cha wiki nzima ya maandamano.
Chanzo cha maandamano hayo yaliyoanzishwa na kizazi cha sasa cha Gen Z mapema wiki hii ni kukithiri kwa ufisadi serikalini mbali na sera duni zinazolenga kukandamiza vijana katika matumizi ya mitandao ya jamii.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Kampeni za uchaguzi mkuu za shika kasi Tanzania

Mgombea wa wadhfa wa Rais wa Jamhurui ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa chama cha Mapinzudi CCM taifa Dkt Samia Suluhu Hasssan anaendeleza kampeni za uchaguzi mkuu kwa chama hicho.
Rais Samia Suluhu, na mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi kutoka chama tawala CCM, wamo katika harakati za kuwashawishi wapiga kura ili kuwachagua kuliongoza taifa hilo kwa awamu nyingine ya miaka mitano ijayo.
Siku ya Alhamis tarehe 11 Septemba 2025, Rais Samia Suluhu alifanya mkutano mkubwa wa siasa katika eneo la Urambo mkoani Tabora, ambako alizungumzia zaidi ufanisi wa maendeleo akisema umetokana na utawala bora wa chama cha Mapinduzi (CCM).
Miongoni mwa hayo ni kuboreshwa kwa muundo misingi ya barabara, afya na ustawi wa uchumi na biashara, na kutaja kimakusudi zao la Tumbaku linalokuzwa kwa wingi mkoani Tabora.
Rais Samia alisema kuwa kunaongezeko kubwa la pato linalotokana na zao la Tumbaku ambapo sasa linauzwa kwa dola 2.5 kutoka bei ya zamani ya dola 1 kwa tani moja.

Kampeni za uchaguzi mkuu nchini Tanzania katika mji wa Urambo mkoa wa Tabora {picha kwa hisani}
Kwa upande wake, Mgombea mwenza Emmanuel Nchimbi alikuwa katika mkoa wa Katavi, kusasambua yale serikali ya Mama Samia Suluhu imepanga kuyatimiza punde tu itakapochaguliwa kuwaongoza Watanzania.
Tanzania inaingia kwenye kampeni za uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba, 29 2025.
Mpinzani wake mkuu Tundu Lissu anaendelea kuzuiwa jela, kwa tuhma za uchochezi na uhaini.
Taarifa ya Eric Ponda