Sports
Mashindano Ya Shule Ya Upili Yaanza Kwa Kishindo Pwani

Mabingwa watetezi wa soka kwa shule za upili eneo la Likoni Moi Forces Academy walianza vyema kampeni ya kutetea taji lao kwa kupata ushindi katika mechi zao zote za makundi.
Katika mechi ya kwanza waliitandika shule ya upili ya Likoni Boyz 2-0 kisha wakawageukia Timbwani na kuwatandika 4-0.
Katika mechi zingine kwenye kundi A, shule ya upili ya Mrima iliitandika Likoni Boys goli 1-0 huku Shikaadabu ikiigaragaza Tibwani magoli 2-0 na kwenye mechi ya pili Mrima ikapigwa magoli 3-1 na Shikaadabu.
Katika kundi B, shule ya upili ya Puma iliilambisha Mwahima magoli 2-1, huku Ushindi ikiilaza Al-Miraj magoli 3-0,nayo Bububu ikipata magoli 2-0 dhidi ya Al- Miraj na katika mechi ya pili Puma ikitoka sare ya 0-0 dhidi ya Ushindi nayo Bubububu ikicharazwa magoli 2-0 na Mwahima.
Katika upande wa akina dada, Kundi A, shule ya upili ya MFGA ilianza vyema kwa kujinyakulia magoli 7-0 dhidi ya Puma, kisha katika mechi ya pili ikaicharazwa na Mishi Mboko magoli 4-0, kisha Mishi Mboko ikailaza Shikaadabu magoli 3-0 na katika mechi ya pili Shikaadabu ikatoka 2-1 dhidi ya Puma.
Katika kundi B, Timwani ilitoka 1-0 dhidi ya Mtongwe Girls, na mechi ya pili Timbwani ikacharazwa 2-0 na Mwahima, nayo Ushindi ikatoka sare ya goli 1-1 na Mwahima, na kisha Mtongwe ikasawazisha mchezo kwa sare ya 0-0 dhihi ya Ushindi.
Kwenye matokeo ya malindi sub county
Barani sec 3-0 Lango BAYA
Canon 0-1 Ganda sec
Barani 1-0 Ganda
Langobaya 2-2 Canon
Malindi 2-0 Bishop Kalu
Gede sec 0-4 Malindi High
Gede 2-0 Bishop Kalu
Sports
Chama Cha Raga KRU Yapata Mwenyekiti Mpya

Chama Cha Raga nchini KRU kimemtangaza Harriet Okach kuwa mwenyekiti mpya kwenye shirikisho hilo kumrithi Sasha Mutai aliyejiuzulu wadhifa wake wiki jana.
Uteuzi huo uliothibitishwa siku ya Alhamisi inamaana kwamba Okach anakua mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti katika Shirikisho hilo la mchezo wa Raga nchini KRU.
Kabla ya kuteuliwa kwake Okach amekua msimazi wa mauzo kwenye shirikisho hilo,na sasa amesema kwamba analenga kuboresha shirikisho hilo na mchezo kwa jumla anachukua hatamu ya uongozi.
“Nataka nichukue fursa hii kuwashukuru nyote kwa kunipa nafasi hii kwanza shirikisho KRU,washikadhau nimeheshimika mno na nimeahidi sitawangusha ,matumaini yangu ni kufanya Mchezo wa Raga na wachezaji wa Raga kuwa katika mandhari mazuri siku za usoni.”
Mutai alijiuzulu wadhifa wake katika Shirikisho hilo kwa kile alichokitaja ni kutopata ungwaji mkono baina ya washikadau wa mchezo huo nchini.
Sports
Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

UEFA NATIONS LEAGUE
Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.
Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.
La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0
Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.
Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.