Connect with us

Sports

Makala ya mbio za magari WRC kufikia Tamati Jumapili Hii

Published

on

Maelfu ya mashabiki kutoka afrika mashariki na kati wamiminika mjini Naivasha kaunti ya Nakuru kwa mbio za magari ya WRC Makala ya mwaka 2025.

Kwa mujibu wa waandalizi Zaidi ya mashabiki 30,000 wametua jijini humo kutoka mataifa ya Uganda,Tanzania na Rwanda kwa mbio hizo ambazo zilianza rasmi siku ya alhamisi jijini Nairobi.

Eflyn Evans dereva kutoka taifa la Wales ndio anaongeza akitumia gari aina ya Toyota Gazoo muda sekunde 46.1 baada ya raundi ya pili akifuatwa na bingwa mara mbili Kalle Rovanpera raia wa uhispania akitumia Toyota pia watatu ni Ottok Tanak raia wa Estonia ambaye anatumia gari aina ya Hyundai Shell Mobis.

Dereva anayeongoza mpaka sasa dereva Eflyn Evans na msaidizi wake Scott Martin alikua na haya yakusema baada ya kuchukua uongozi wa mapmea.

“Plan yetu ilifanya kazi vizuri,tunafuraha kuchukua uongozi wa mapema ila bado kazi ipo kwani mizungumzo ni minane,tutaona itakavyokua mpaka siku ya mwisho.”

Kwa upande wake dereva nambari mbili na bingwa mtetezi Kalle Rovanpera na msaidizi wake Jonne Halttunen alisema haya baada ya kushindwa;

“Leo haikua siku nzuri kwetu tulitumia muda mwingi asubuhi ila bado safari ya sisi kurejea kileleni.”

Naye dereva namba tatu Ott Tanak aliyasema haya;

“Hauwezi ukapanga kusema kweli ukiwa hapa kenya vitu vingi vinafanyika,Ni lazima tuketi chini tufahamu tatizo ambalo linatukumba na gari letu.”

Raundi ya tatu na nne yanaishwa maeneo ya Elmentaita huku jumapili mbio hizo zikiisha Hells Gate 1 na Hells GATE 2.

Kilele cha mbio hizo ni siku ya jumapili ambapo rais William Samoei Ruto anatarajiwa kufunga mbio hizo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Taifa Ya Nigeria Super Falcons Imepokea Zawadi Nono Kutoka Kwa Rais

Published

on

By

 Mabingwa wa Bara Afrika kwa soka la akina dada Super Falcons wamevuna vinono kutoka kwa rais wa taifa hilo punde tu baada ya kutua kutoka mjini Rabat Morocco.
Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu akitangaza zawadi zifuatazo kwa timu ya Super Falcons:
Kila mchezaji atapokea dola 100,000 za Kimarekani
Kila mchezaji atapewa nyumba ya vyumba vitatu
Kila mwanachama wa benchi la ufundi atapokea dola 50,000 za Kimarekani
Zaidi ya hayo, Jukwaa la Magavana wa Nigeria limewazawadia kila mchezaji kiasi cha ₦10 milioni (takriban dola 6,000 za Kimarekani).
Vipusa hao waliwashinda wenzao wa Morocco magoli 3-2 kwenye fainali kali iliosakatwa siku ya Jumamosi na kutwa ubingwa huo likiwa ni taji lao la kumi katika historia ya kombe hilo.
Continue Reading

Sports

Morocco Waanza Mazoezi Nyayo Tayari Kwa CHAN

Published

on

By

SIKU 4 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN
Timu ya Taifa Ya Morocco marufu ‘Atlas Lions ‘ wamefanya mazoezi Yao ya kwanza Ugani Nyayo hapo jana kujinoa tayari kwa mechi ya ufunguzi.
Vijana hao waliwasili mapema Jana tayari kwa kipute hicho kinachongoa nanga Jumamosi hii ugani Benjamin Mkapa nchini Tanzania.
Badhi ya wachezaji nyota kwenye kikosi hicho ni pamoja na;mshambulizi El Mahraoui Anas pamoja na kiungo Khairi Ayoub wa RS Berkane.
Hii hapa ni kikosi chote cha Taifa hilo kwa kombe la CHAN;
Magolikipa:
  • Al Harrar Elmehdi
  • Rachid Ghanimi (FUS Rabat)
  • Aqzdaou Omar (Wydad Casablanca)

Mabeki:

  • Moufid Mohamed (Wydad Casablanca)
  • Boulacsout Mohamed
  • Mchakhchekh Mehdi
  • Louadni Marouane
  • Arrassi Bouchaib
  • Assal Abdelhak (RS Berkane)
  • Belammari Youssef (Raja Casablanca)
  • Zahouani Fouad

Viungo:

  • Khairi Ayoub (RS Berkane)
  • Hrimat Mohamed Rabie
  • Souane Amine
  • Essadak Houssam
  • Hajji Reda (RS Berkane)
  • Bach Anas
  • Aït Ouarkhane Khalid
  • Bougrine Sabir

Washambulizi:

  • Mehri Youssef (RS Berkane)
  • El Mahraoui Anass
  • Bouhra Saïf-Eddine (Wydad Casablanca)
  • Baba Khalid
  • Riahi Imad (RS Berkane)
  • Salaheddine Errahouli
  • Mouloua Ayoub
  • El Kaabi Youness
  • Lamlioui Oussama (RS Berkane) Morocco wanafungua kampeini Yao dhidi ya Angola siku ya Jumapili Ugani Nyayo kwenye kundi A.
Continue Reading

Trending