Connect with us

News

Mahakama ya Mombasa kusikiza kesi ya ulawiti Septemba 8

Published

on

Mkufunzi wa mchezo wa soka kaunti ya Mombasa Mbarak Swaleh maarufu Coaches amefikishwa katika Mahakamani ya Mombasa akikabiliwa na kosa la ulawiti wa mtoto wa kiume wa umri wa miaka 12 ambaye ni mchezaji katika timu anayoifunza.

Mahakama ilielezwa kwamba Swaleh alitekeleza kitendo hicho kati ya mwezi Januari na Agosti 14, 2025, katika eneo la uwanja wa soka wa Fort Jesus katika eneo bunge la Mvita.

Mahakama pia ilielezwa kwamba mshukiwa alimshawishi mtoto huyo hadi kwenye chumba cha kuhifadhi vifaa vya soka kwa kisingizio cha kuchukua vifaa vya mazoezi kisha akamdhulumu kimapenzi.

Aidha, kocha huyo pia anakabiliwa na shtaka lengine la kutekeleza kitendo kichafu kwa mtoto huyo ambapo tukio hilo lilifichuliwa na mtoto mwenyewe mnamo tarehe 16 Agosti, 2025 baada ya kumueleza mamake mzazi kuhusu unyanyasaji huo.

Akiwa mbele ya Hakimu mkaazi mwandamizi David Odhiambo mshukiwa alikana mashtaka dhidi yake na akaachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki tano pamoja na mdhamini wa kiasi sawa hicho.

Kesi hiyo itatajwa tena mnamo Septemba 8 mwaka huu.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Maandalizi ya Maadhimisho ya Chenda Chenda

Published

on

By

Ni dhahiri sasa kutakuwa maaadhimisho ya Chenda Chenda siku ya Jumanne Septemba 9, 2025 kwa wakati mmoja katika kaunti ya Kwale na kaunti ya Kilifi.

Waasisi wa maadhimisho haya ambao ni wWazee wa kutoka Kaya zote za Wamijikenda walitangaza mwaka uliopita kwamba maadhimisho ya mwaka huu yafanyika katika kaunti ya Kwale baada ya kuandaliwa eneo la Kaya fungo kaunti ya Kilifi mwaka jana.

Na baada ya vikao vya mashauriano baina ya Wazee wa Kaya zote hivi majuzi katika eneo la Rabai, Wazee hao waliafikiana kwa kauli moja kwamba maadhimisho hayo ya mwaka huu yaandaliwe katika Kaya ya Mtswakara eneo bunge la Kinango katika Kaunti ya Kwale.

Lakini baada ya tangazo hilo kutolewa, serikali ya kaunti ya Kilifi ilitangaza kufanya maadhimisho hayo katika uwanja wa chuo kikuu cha Pwani.

Tangazo hilo liliwaghadhabisha mno Wazee wa Kaya ambao katika taarifa kwa Wanahabari walisema wanaendelea na mipango ya maadhimisho hayo katika kaunti ya Kwale.

Maandalizi ya Maadhimisho ya Chenda Chenda, kaunti ya Kilifi

Hali hii imezua tofauti kubwa baina ya Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Maitha Mung’aro anayedaiwa kuenda kinyume na utaratibu wa tamaduni za Kaya, ambapo maadhimisho hayo yanapasa kufanyika katika viwanja vya Kaya kama njia moja ya kuwaheshimu wavyele wa Kaya za Kimijikenda.

Huku hayo yakijiri maandalizi ya maadhimisho hayo yanaendelea katika uwanja wa Chuo kikuu cha Pwani.

Wazee wa Kaya wanalaumu kitendo hiki na kuongeza kwamba maandalizi haya yanamsukumo wa kisiasa na wala sio ule wa kitamaduni na unaokusudiwa kuleta umoja wa Wamijikenda.

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading

News

Jopo la kushughulikia fidia kwa waathiriwa wa maandamano laanza kazi

Published

on

By

Jopo lililoundwa na Rais William Ruto kushughulikia masuala ya fidia ya waathiriwa wa ukatili wa polisi wakati wa maadamano limeanza kikao cha wiki moja huku mjadala kuhusu uhalali na uwazi wa jopo hili ukitiliwa shaka na kupokea upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu na viongozi wa upinzani.

Jopo hilo linaongozwa na Prof. Makau Mutua na naibu wake Rais wa Chama cha Wanasheria nchini (LSK), Faith Odhiambo, ambaye uteuzi wake umeibua mjadala mkali.

Baadhi ya Wanasheria walimshutumu Odhiambo kwa “kusaliti haki,” lakini yeye alisisitiza kwamba jukumu lake ni kuhakikisha waathiriwa wa ukatili wa polisi wanapata haki waliyoikosa kwa muda mrefu.

Aliongeza kuwa jopo hilo lina nafasi ya kuleta mabadiliko ya kihistoria katika upatikanaji wa fidia kwa waathiriwa.

Kwa mujibu wa maelezo yake, jopo hilo si tume ya kikatiba wala chombo cha kisheria chini ya Katiba, bali ni jopo la ushauri lililoanzishwa na Rais chini ya Kifungu cha 132(4)(a).

Vile vile alibainisha kuwa wanachama wa jopo hilo si maafisa wa umma hivyo uteuzi wao hauhitaji mchakato wa Tume ya Utumishi wa Umma kwa mujibu wa Kifungu cha 260 cha Katiba.

Jopo lililoundwa na Rais William Ruto kushughulikia ya fidia ya waathiriwa wa maadamano

Hata hivyo, wakosoaji walisema linaweza kukiuka mamlaka ya ofisi huru kama Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP), Inspekta Jenerali wa Polisi na Tume ya Kitaifa ya Haki za Binadamu (KNCHR). Jopo hilo limekanusha madai hayo, likisema jukumu lake ni kusaidia na sio kuchukua nafasi ya taasisi zilizopo.

Wapo pia wanaouliza uhalali wa serikali kuwalipa fidia waathiriwa ilhali serikali hiyo hiyo imeshtumiwa kwa mauaji, kutoweka kwa baadhi ya wakosoaji wa serikali kwa njia tatanishi na kuacha familia na majeraha yasiyotibika.

Jopo hilo pia linasisitiza kikatiba, serikali ndiyo chombo kinachobeba wajibu wa kurekebisha madhila kwa niaba ya taifa. Hata kama madhara yalisababishwa na maafisa wa serikali, haitazuiwa kuwafidia waathiriwa.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

Trending