News
Lazima Tufunge Tunisia Magoli ya Mapema, Kauli ya Kocha Odemba Kuelekea Mechi ya Starlets

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee starlets Beldine Odemba ana amini kwamba uwepo wa mashabiki katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex Ijumaa hii itawapa msukumo timu hiyo wanapojianda kwa mechi ya kufuzu dimba la Afrika AWCON mwakani.
Akizungumza na wanahabari Odemba amesema anasubiri mchezaji wa mwisho kambini Jumatano hii.
“Tuko na karibu full house baada kuwasili kwa wachezaji zaidi ya kumi wa kulipwa,Tunasubiri mchezaji wa mwisho Jumatano hii.” Kocha anazidi kuelezea kwamba, “Lengo letu ni kushinda Tunisia hapa Nyumbani kabla ya mechi ya mkondo wa pili mjini Tunisia Feb 26. Kwa mujibu wa mwalimu huyo na kikosi mchanganyiko Yani chipukizi na wazoefu inampa msukumo kwamba tutaandikisha matokeo chanya, “Wachezaji chipukizi ndio Harambee starlets ya badaye kuwepo kwao kambini inanisaidia kuwa na upana wa kikosi na kujenga kikosi Cha usoni vile vile.Kwa upende wake kiungo wa Besikitas ya Uturuki Cynthia Shilwatso ni kwamba hawataki kujuta Tena baada ya kubanduliwa na Botswana mwaka Jana,” Lengo Letu ni kushinda nyumbani ndio tuenjoy mchezo ugenini, Ni lazima tufunge Tunisia magoli ya mapema kilichotupata mwaka Jana kisitupate tena.”
Kambi ya Harambee starlets imekamilika baada ya wachezaji wa kigeni wote kuwasili kwa pambano la kufuzu dimba la AWCON dhidi ya Tunisia Ijumaa hii ugani Ulinzi Sports Complex mjini Nairobi.
Mechi hiyo itapigwa majira ya saa tisa kiingilio ni shs. 100 mashabiki wa kawaida na shs. 500 watu mashuhuri (VIP).
News
Chama cha DCP chashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025/26.

Uongozi wa chama cha DCP chake Rigathi Gachagua sasa unashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025/26 ukidai unavipengee tata vitakavyoongeza mzigo wa ushuru kwa wakenya.
Kulingana na naibu kinara wa chama hicho Cleophas Malala mswada huo hauzingatii hali ya uchumi kwa wakenya ambao wanaendelea kukabiliana na gharama ya juu ya maisha.
Malala alitaja baadhi ya vipee vinavyoibua maswali kama vile kodi mpya ya kuongezwa kwa ushuhru wa VAT kwenye bidhaa za kawaida kama vile vyakula.
Akizungumza mjini Mombasa Malala alishauri wakenya kuwa makini na kushiriki mchakato wa kuchambua mswada huo kikamilifu vile vile kutoa maoni kwa bunge kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.
Vile vile Malala alimlaumu kinara wa chama cha ODM Raila Odinga pamoja na Rais William Ruto akidai wamehadaa familia zilizowapoteza wapendwa wao mwaka jana wakati wa kupinga mswada wa fedha kwamba zingefidiwa.
Taarifa ya Joseph Jira.
News
Mamlaka ya KPA yalalamikia changamoto zinazolemaza shughuli zake.

Licha ya Bandari ya Mombasa kuendelea kurekodi matokeo bora katika utendakazi wake,mamlaka ya bandari nchini (KPA) imebainisha kwamba bado kuna changamoto zinazolemaza shughuli zake.
Akizungumza katika kikao na kamati ya bunge kuhusu ushirikiano wa kikanda, mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya KPA, Nahodha William Ruto, alieleza kuwa changamoto hizo ni pamoja na idadi kubwa ya mashirika yanayokagua mizigo, vizuizi vya kupima uzito wa magari (weighbridges), na vizuizi vya polisi barabarani katika eneo la Kaskazini (Northern Corridor).
Kulingana na nahodha Ruto hali hiyo bado inaathiri ufanisi wa usafirishaji wa mizigo na biashara kwa ujumla.
Nahodha Ruto pia alieleza athari za ada zisizo rasmi zinazotozwa na mashirika mbalimbali, pamoja na ushuru wa CESS unaotozwa na serikali za kaunti kwa mizigo ambayo tayari imekaguliwa na kulipiwa bandarini.
Aliongeza kuwa gharama hizo za ziada zinaathiri ushindani wa Kenya kama kitovu cha biashara katika ukanda wa afrika mashariki.
Wakati uo huo, Ruto aliitaka serikali kuharakisha uboreshaji wa mifumo ya usafirishaji kwa kuongeza matumizi ya teknolojia na kuunganisha mifumo ya upimaji wa uzito wa magari kote nchini.
Kwa upande wake, kamati ya bunge kupitia kwa mwenyekiti wake, Bi. Irene Mayaka, iliahidi kwamba kamati hiyo itafuatilia kwa karibu malalamshi yaliyoibuliwa na kuhakikisha kwamba suluhu mwafaka inapatikana.
Taarifa ya mwanahabari wetu.