News
Lazima Tufunge Tunisia Magoli ya Mapema, Kauli ya Kocha Odemba Kuelekea Mechi ya Starlets

Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee starlets Beldine Odemba ana amini kwamba uwepo wa mashabiki katika uwanja wa Ulinzi Sports Complex Ijumaa hii itawapa msukumo timu hiyo wanapojianda kwa mechi ya kufuzu dimba la Afrika AWCON mwakani.
Akizungumza na wanahabari Odemba amesema anasubiri mchezaji wa mwisho kambini Jumatano hii.
“Tuko na karibu full house baada kuwasili kwa wachezaji zaidi ya kumi wa kulipwa,Tunasubiri mchezaji wa mwisho Jumatano hii.” Kocha anazidi kuelezea kwamba, “Lengo letu ni kushinda Tunisia hapa Nyumbani kabla ya mechi ya mkondo wa pili mjini Tunisia Feb 26. Kwa mujibu wa mwalimu huyo na kikosi mchanganyiko Yani chipukizi na wazoefu inampa msukumo kwamba tutaandikisha matokeo chanya, “Wachezaji chipukizi ndio Harambee starlets ya badaye kuwepo kwao kambini inanisaidia kuwa na upana wa kikosi na kujenga kikosi Cha usoni vile vile.Kwa upende wake kiungo wa Besikitas ya Uturuki Cynthia Shilwatso ni kwamba hawataki kujuta Tena baada ya kubanduliwa na Botswana mwaka Jana,” Lengo Letu ni kushinda nyumbani ndio tuenjoy mchezo ugenini, Ni lazima tufunge Tunisia magoli ya mapema kilichotupata mwaka Jana kisitupate tena.”
Kambi ya Harambee starlets imekamilika baada ya wachezaji wa kigeni wote kuwasili kwa pambano la kufuzu dimba la AWCON dhidi ya Tunisia Ijumaa hii ugani Ulinzi Sports Complex mjini Nairobi.
Mechi hiyo itapigwa majira ya saa tisa kiingilio ni shs. 100 mashabiki wa kawaida na shs. 500 watu mashuhuri (VIP).
News
Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.
Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.
Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro
Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.
Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.
Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.
Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.
‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.
Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.
Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.
Taarifa ya Janet Mumbi
-
Entertainment9 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment21 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News18 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni