Connect with us

Sports

Kikosi Cha Handiboli Ya Ufukweni Yajinoa Tayari Kwa Kombe La Dunia

Published

on

Katibu Mkuu ambaye pia ni msimamizi wa mchezo wa Handiboli ya Ufukweni (Beach Handball) ya Kitaifa Bi Carolyne Nyadiero amesema kwamba mandalizi yamekamilika kwa ajili ya safari yao ya kuelekea Tunisia wikendi hii.

Akizungumza na Kipenga cha Coco Fm Bi Nyadiero amesema kwamba malengo yao ni kumaliza wa kwanza Barani Afrika na kufuzu Olimpiki Mwaka 2026 kule Dakar Senegal.

“Nataka nishukuru Mungu pili nishukuru gavana wa kaunti hii na washikadhau ikiwemo Rais wa chama cha mchezo huu na waziri wa michezo ambao wametushika mkono tangu tulipopokea barua ya mashindano haya,Lengo letu ni kushinda ubingwa na kushiriki olimpiki 2026 nchini Senegal.

Kwa upande wake kocha wa kikosi cha wanaume Boaz Maroko amesema kwamba mandalizi ya kikosi hicho yamekua mazuri na wanalenga kushinda kombe hilo ama kuwa bora barani afrika.

“Tumejiandaa tangu mwaka jana na vijana wako katika hali shwari tunataka wa kwanza barani afrika kando na kushinda ubingwa wa kombe hili la dunia.”

Ni kauli ambayo imeweza kuungwa mkono na kocha wa kikosi cha akina dada Titus Kasekwa.

“Tumejiandaa vizuri zaidi Makala yaliyopita tulipata silver ila mwaka huu tunataka kupata tuzo kuu na kunyakua dhahabu kwenye mashindano haya.

Kikosi hicho kinakamilisha mazoezi yake siku ya Ijumaa kabila kuondoka Jumamosi kwa kombe la dunia nchini Tunisia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending