National News
KEMSA Yazitaka Kaunti Kulipa Malimbikizi ya Madeni ya Jumla ya Shilingi Bilioni 3.5

Mamlaka ya kusambaza dawa nchini KEMSA imezitaka serikali za kaunti kulipa malimbikizi ya madeni ya jumla ya shilingi bilioni 3.5 zinazodaiwa na Mamlaka hiyo.
Kulingana na Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo ya KEMSA, Dkt. Waqo Ejersa, madeni hayo ambayo yamekaa kwa mda sasa yanaathiri utendakazi wa mamlaka hiyo.
Akizungumza na Wanahabari jijini Mombasa baada ya kikao kilichowaleta pamoja wakuu wa KEMSA, Dkt. Ejersa amesema iwapo madeni hayo yatalipwa kwa wakati basi itasaidia Mamalaka hiyo kusambaza dawa kwa wakati hospitalini.
Kauli yake ikiungwa mkono na Mwenyekiti wa bodi ya KEMSA nchini Samuel Tunai, ambaye amesema Mamlaka hiyo imeweka mikakati ya kuhakikisha hospitali za umma nchini zinakuwa na dawa na vifaa vya kutosha huku akisema mpango wa SHA unaendelezwa vyema.
National News
Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).
Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa
Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.
Taarifa Ya Elizabeth Mwende
National News
Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.
Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.
Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.
Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.
Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.
Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.
Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.
Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.
Taarifa ya Joseph Jira
-
Entertainment9 hours ago
Mbilia Bel Anusurika Kwenye Ajali ya Barabarani – Kinshasa
-
Entertainment21 hours ago
#COCODRIVE: Crack Sound Siyo Mashine, Ni Vichwa – J Crack Asema Baada ya Kuibiwa Vyombo Studioni Kwake
-
International News18 hours ago
Mgombea wa urais wa ACT wazalendo Luhaga Mpina, arejeshwa debeni