Connect with us

News

KDF kujigharamia chakula chao cha mchana.

Published

on

Wanajeshi nchini sasa watalazimika kujigharamia chakula chao cha mchana kuanzia Julai mosi mwezi ujao.

Hii ni baada ya serikali ya Rais William Ruto kusisitiza kuwa itafutilia mbali mpango wa ruzuku ya chakula kwa wanajeshi.

Hatua hiyo imezua taharuki miongoni mwa maafisa wa jeshi la ulinzi la Kenya yaani KDF hasa wale wa ngazi za chini wanaotegemea pakubwa mpango huo wa serikali.

Mpango huo wa chakula cha mchana uliokuwa ikifadhiliwa na hazina ya serikali kwa maafisa hao sasa utachulikwa na mfumo mpya wa lipa unapokula yaani “Pay as you Eat”.

Badhi ya maafisa wa vyeo chini walilalamika wakidai tayari wanabeba mzigo mzito wa kifedha kama vile mikopo huku wakisema wanahofu huenda wakalazimika kuwacha kula kabisa chini ya mpango huo mpya.

Kulingana na wizara ya ulinzi kufutilia mbali chakula hicho cha bila malipo ni njia ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kuwapa wanajeshi uhuru wa kuchagua wanachokula.

Vile vile wizara hiyo inasema fedha zilizokuwa zikitumika kwa mfumo wa sasa zitatumika kuboresha miundombinu ya maeneo ya chakula, ununuzi wa vifaa vya upishi na kulipa madeni ya chakula yaliyosalia.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending