Business
Kaunti ya Kilifi yaendeleza mikakati ya kuimarisha sekta ya uvuvi

Mkurugenzi wa masuala ya uvuvi kaunti ya Kilifi Mwangi Gachuru amesema serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mikakati katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwenye kaunti hii ya Kilifi.
Gachuru alisema wanashirikiana na wasimamizi wa fuo za bahari katika kaunti ya Kilifi katika kuhakikisha wavuvi wananufaika kupitia raslimali za baharini.
Aidha, Gachuru aliwahimiza wavuvi na wenyeji wa kaunti ya Kilifi kushirikiana ipasavyo kuhakikisha raslimali hizo zinawafaidi ipasavyo.
“Ni kupitia ushirikiano pekee ndipo mtaweza kuendeleza uvuvi wenu vizuri’’, alisema Gachuru
Akizungumzia mzozo baina ya wavuvi, Gachuru aliwataka kuzingatia sheria zilizopo kwa mujibu wa sheria za uvuvi ili kupatikane mwafaka na sio kuchukua sheria mkononi na kuahidi kuwa watawakabili kisheria wale ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku kutumika baharini kuvua samaki.
“Panapotokea ugomvi miongoni mwenu, zingatieni sheria na sio kuchukua sheria mkononi’’ Aliongeza Gichuru.
Taarifa ya Janet Mumbi
Business
Wafanyibiashara wa Shanga wavuna kutokana na watalii Mombasa

Wafanyibiashara kaunti ya Mombasa wanaendelea kuvuna zaidi kutokana na watalii wa ndani na nje waliozuru kaunti hiyo kufuatia maonyesho ya kimataifa ya Kilimo ambayo yalikamilika siku ya Jumapili.
Kulingana na wafanyibiashara wa kuuza shanga eneo la Lights kaunti ya Mombasa walisema idadi ya watalii ambao walitembelea eneo hilo imefanya biashara kuimarika.
Wakizungumza na CocoFm, walisema bei za Shanga zilipanda kutoka shilingi mia tatu hadi mia tano kwa shanga ndogo huku shanga kubwa zikiuzwa kwa shilingi elfu moja
Hata hivyo waliitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuimarisha usalama katika maeneo mengi ya kaunti hiyo ili kuwavutia watalii zaidi.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Kenya kuzindua utalii wa anga (Astro-tourisim)

Kenya itakuwa mwenyeji wa uzinduzi wa utalii wa anga(Astro-tourisim) katika kaunti ya Samburi Septemba 7, 2025, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha na kubadilisha aina za utalii nchini.
Uzinduzi huo unaendana sambamba na tukio la mwezi kupatwa maarufu kama Blood moon ambapo litaanza saa mbili na nusu usiku wa septemba 7, 2025, na kudumu kwa dakika 82.
Mpango huu wa kipekee unalenga kuifanya Kenya kuwa kivutio kikuu cha wapenzi wa sayansi ya anga na wasafiri wa kimataifa wanaopenda maajabu ya siri.
Kwa mujibu wa shirika la Magical Kenya, tajriba hii ya anga inalenga kutumia mazingira ya kipekee ya nchi kufungua ukurasa mpya na endelevu wa utalii.
Waziri wa utalii na wanyama pori Rebecca Miano atakuwa mgeni rasmi akiandamana na wageni wa kimataifa katika hafla hiyo itakayofanyika katika Sopa Lodge kwenye hifadhi ya kitaifa ya Samburu.
Taarifa ya Joseph Jira