Connect with us

Business

Kanda ya Pwani kuimarika kupitia Kilimo cha kisasa

Published

on

Kanda ya Pwani inatarajiwa kuimarika zaidi kupitia Kilimo cha kisasa kinachotekelezwa kupitia mfumo wa teknolojia.

Hii ni kupitia mikakati inayoendelezwa na Agitech Seedlings kuhakikisha Wakulima na Wenyeji wa Kanda ya Pwani wanakumbatia Kilimo cha kisasa kama maeneo mengine nchini.

Akizungumza na Coco FM katika maonyesho ya Kilimo cha kisasa na uzinduzi wa tawi jipya la Agitech Seedling katika eneo la Kwa Ndomo mjini Malindi kaunti ya Kilifi, Mkurugenzi wa Agitech Seedlings Peter Karanja Ndung’u alieleza sababu za kuanzisha Kilimo hicho cha kisasa katika ukanda wa Pwani.

Karanja pia alisema wanapania kuhakikisha wenyeji wa Pwani wanahamasishwa ipasavyo na hata kuonyeshwa namna ya kufanya Kilimo hicho hapa pwani.

“Kupitia hamasa ambazo tunatoa kwa wakulima na wenyeji wa Pwani kwa jumla tunatarajia kuwa Kilimo kitaanza kuimarika na kuondoa dhana ambayo imekuwepo kwamba eneo la Pwani linatambulika pekee kwa masuala ya uvuvi’’, alisema Karanja.

Vilevile, Karanja alisema kuna haja ya Wakulima kutunza ardhi zao kwa kuhakikisha zina rutuba ya kutosha ili kuzalisha chakula kwa wingi na bora.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Mradi wa kiuchumi wa Dongo Kundu wavutia wawekezaji zaidi

Published

on

By

Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi wanaendelea kuonyesha nia ya kuekeza katika mradi wa kiuchumi wa dongo kundu kaunti ya Mombasa.

Mradi huo unaotarajiwa kuongeza uzalishaji katika viwanda na thamani ya bidhaa ndani ya nchi na nje, unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.

Kampuni ya nishati kutoka China, Ruike Energy Group Limited, ni mwekezaji wa hivi karibuni kuonyesha nia ya kupata nafasi ndani ya eneo hilo la kiuchumi la Dongo Kundu kwa ajili ya kuanzisha kiwanda cha kusafisha mafuta.

Kulingana na halmashauri ya bandari nchini KPA hatua hiyo italeta faida Zaidi ikiwemo kubuni nafasi za ajira, ikuaji wa uchumi, upatikanaji wa vifaa vya baharini, na urahisi wa kufikia masoko ya kanda na ya kimataifa.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

KETRACO kuimarisha usalama wa chakula nchini

Published

on

By

Shirika la usambazaji umeme nchini, KETRACO, limethibitisha dhamira yake ya kuimarisha usalama wa chakula, ukuaji wa kijani, na ushirikiano wa kieneo kupitia uekezaji mkubwa katika miundombinu ya umeme.

Katika maonesho ya Kimataifa ya kilimo ASK yanayoendelea kaunti ya Mombasa, KETRACO imeonyesha jinsi miundombinu yake ya umeme inavyowezesha kilimo cha kisasa na uzalishaji wa viwandani.

Kwa mujibu wa kaimu mkurugenzi mkuu, mhandisi Kipkemoi Kibias, KETRACO imekamilisha miradi 43 ya njia za kusafirisha umeme, huku mingine 29 ikitarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2028.

Kibias, alisema shirika hilo tayari limejenga zaidi ya kilomita elfu sita za njia za umeme wa msongo mkubwa, likiwa pia na vituo 46 vya kusambaza umeme na upanuzi wa mitambo 33.

Katika eneo la Pwani, Kibias alisema upanuzi wa mpango wa Green Energy Backbone umewezesha usambazaji wa kawi safi kwa asilimia 93, jambo lililopunguza utegemezi wa mafuta na kuchochea maendeleo ya biashara za kilimo, utalii na uchumi wa baharini.

Kibias alisema KETRACO inaendelea kuwekeza katika teknolojia za kisasa na kuunganisha Kenya na nchi jirani kupitia njia za kimataifa kama zile za Ethiopia, Tanzania na Uganda hatua zitakazowezesha biashara ya umeme Afrika Mashariki.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending