Connect with us

News

Kalonzo:Rais Ruto ajiondoe mamlakani.

Published

on

Kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka amemshauri rais William Ruto kuondoka madarakani pamoja na serikali yake ili kupisha mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa kitaifa.

Kalonzo alisema yanayoendelea nchini kwa sasa yamedhihirisha wazi namna idadi kubwa ya wakenya ambavyo hawaridhishwi na uongozi rais Ruto.

Kalonzo alidokeza kuwa taifa linaongozwa kwa misingi ya sheria na demokrasia, hivyo hakuna makosa kwa wakenya kuwakosoa viongozi walio madarakani vile vile kueleza hisia zao.

Kinara huyo alisema wito wa viongozi wa kanisa nchini wa kushinikiza mazungumzo ya kitaifa unafaa kuzingatiwa na kuhakikisha mazungumzo hayo yanahusisha pande zote husika.

Aliongeza kuwa kunaumuhimu wa serikali kusikiliza malalamishi ya vijana wa kizazi cha Gen Z, vile vile kuhakikisha maafisa wa usalama wanawapa Gen Z ulinzi wakutosha wakati wanapofanya maandamano mbali na kuwadhuru.

“Mambo ya Gen Z ni suala muhimu kabisa, lakini wakifanya maandamano ni lazima serikali ihakikishe ni maandamano ya amani, usije kupiga watoto risasi, unawauwa halafu unawalaumu, haifai”.alisema Kalonzo.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending