Entertainment
#JP2025: Mavazi ya Diamond Harusini kwa Jux Yaibua Gumzo

Msanii maarufu wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ameibua mjadala mkali kwenye harusi ya kifahari ya Juma Jux na Priscilla Ojo iliyofanyika nchini Tanzania, baada ya kushindwa kufuata mavazi rasmi yaliyowekwa kwa hafla hiyo.
Alfajiri ya Alhamisi, Juma Jux alitoa ujumbe wa kukumbusha wageni wake wote kuhusu kuzingatia mavazi rasmi ya harusi hiyo: nyeusi na dhahabu.
Hata hivyo, wakati wa hafla ya mapokezi, Diamond alijitokeza akiwa amevalia suti nyeupe – akiwa ndiye mwanamume pekee aliyekiuka mwongozo wa mavazi uliotolewa.
Tukio jingine lililovutia hisia za wengi ni kutowasili kwake kwenye harusi hiyo pamoja na mpenzi wake, Zuchu.
Zuchu alifika peke yake katika hafla hiyo ya kifahari, huku Chibu Dangote (Diamond) akichelewa kufika. Hali hiyo ilizua maswali zaidi baada ya wawili hao kuketi kwenye meza tofauti, jambo lililowafanya mashabiki wao kuanza kuhusisha tukio hilo na tetesi za mgogoro kati yao.
Katika toleo la sita la harusi ya Juma Jux na Priscilla lililofanyika awali nchini Nigeria, Diamond alikuwa msimamizi mkuu (Best Man), lakini kwa hafla ya usiku iliyofanyika hivi karibuni, nafasi hiyo ilichukuliwa na msanii mwingine, Billnass.
Harusi ya Kipekee
Priscilla Ojo, binti wa muigizaji maarufu wa Nollywood Iyabo Ojo, alifunga ndoa na Juma Jux katika kile kinachotajwa kuwa mojawapo ya harusi zinazozungumziwa zaidi mwaka huu.
Sherehe hiyo, iliyopewa jina la utambulisho wa mtandaoni #JP2025, ilikuwa tamasha la kiutamaduni lililopambwa kwa shamrashamra, hisia nzito, mastaa wakuu, na mitindo ya kuvutia kutoka pande zote.
Safari ya wawili hao ilianza miezi kadhaa iliyopita, kupitia sherehe ya utambulisho iliyofanyika nchini Tanzania mwezi Februari, ambapo ndugu na marafiki wa karibu walikusanyika kushuhudia mwanzo wa safari yao ya ndoa.
Lakini Jux hakuishia hapo. Kabla ya Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day), alifanya pendekezo jingine la ndoa, safari hii akimvisha pete ya almasi ya karati 5.2 — tukio lililowaacha wengi wakiwa na hisia kali mitandaoni, na kuthibitisha kuwa uhusiano wao umejengwa juu ya upendo wa kweli.
Baada ya hapo, wawili hao walifunga ndoa ya kiserikali (civil wedding) jijini Lagos nchini Nigeria.
Kisha, tarehe 17 Aprili 2025, Priscilla na Juma waliandaa harusi ya kitamaduni katika hoteli moja ya kifahari iliyoko eneo la Oniru, Nigeria. Hafla hiyo ilikuwa muunganiko mzuri wa tamaduni za Nigeria na Tanzania, ambapo kila hatua ya sherehe hiyo ilikuwa na uzito wake wa kihistoria.
Jumamosi, tarehe 19 Aprili 2025, wapenzi Juma Jux na Priscilla Ojo waliidhinisha rasmi muungano wao kwa mara nyingine kupitia harusi ya kuvutia ya kanisani (white wedding) iliyofanyika jijini Lagos, Nigeria.
Msanii nyota kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, aliteuliwa kuwa msimamizi wa harusi (Best Man), huku mwanamitindo na mshawishi wa mitandao ya kijamii, Diana Eneje, akiwa msimamizi wa bibi harusi (Best Maid).
Hafla hiyo ilihudhuriwa kwa wingi na mastaa mbalimbali kutoka tasnia ya filamu ya Nollywood na muziki, na kuwa tukio la kijamii lililoangaziwa sana na vyombo vya habari.
Miongoni mwa watangazaji wa hafla hiyo alikuwa Claudia Naisabwa kutoka Kenya. Wageni maarufu waliokuwepo pia walijumuisha Chioma Ikwokwu, Funke Akindele, rafiki wa karibu wa Priscilla Prince Enioluwa Adeoluwa kutoka Nigeria, pamoja na Raza Lee kutoka Tanzania, miongoni mwa wengine wengi waliopamba tukio hilo la kifahari.
Entertainment
Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua
Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.
Kwenye Facebook, Yena, aliandika:
“We give God all the Glory. #Ametutendea”
Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨
🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”
Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.
👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)
Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!
💍 Safari ya Upendo Yao
Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!
Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:
“AMETUTENDEA!” 🎉
📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.
Entertainment
Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien
Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.
Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!
Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.
Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.
Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.
Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.
Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.
Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.