Sports
Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.
Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.
Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.
“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”
Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG
Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.
Sports
Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.
Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.
Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.
Sports
Winga Wa Colombia Luis Diaz Sasa Ni Mali Ya Bayern

Klabu ya Bayern Munich, inayoshiriki Ligi Kuu ya Bundesliga nchini Ujerumani, imetangaza kumsajili winga wa Colombia, Luis Díaz.
Hatua hii imekuja baada ya Bayern Munich na Liverpool kufikia makubaliano kuhusu uhamisho wa mchezaji huyo kwa ada ya pauni milioni 65.5.
Díaz, mwenye umri wa miaka 28, aliwasili mjini Munich hapo jana kwa ajili ya vipimo vya kitabibu kabla ya kutia saini mkataba wa miaka minne na mabingwa hao wa Ujerumani.
Mchezaji huyo alijiunga na Liverpool mwaka 2022 akitokea klabu ya Porto kwa ada ya pauni milioni 37. Tangu wakati huo, ameifungia Liverpool mabao 41 katika mechi 142 alizocheza uwanjani Anfield.
Nyota huyo aliondoka kwenye kambi ya mazoezi ya Liverpool mjini Hong Kong hapo jana na kujiunga rasmi na waajiri wake wapya kwa maandalizi ya msimu mpya.