Connect with us

News

Gor Mahia Yailaumu Fkf Kutokana Na Vurugu Gusii

Published

on

Mabingwa mara 21 ligi kuu humu nchini kilabu ya Gor Mahia imeilaumu shirikisho la soka nchini FKF pamoja na kamati inayosimamia ratiba ya mechi za ligi kuu kutokana na vurugu iliyoshuhudiwa ugani Gusii wikendi.

Kupitia barua kilabu hiyo imelaani kitendo hicho huku ikisema kwamba shirikisho pamoja na wasimamizi wa ligi hiyo waliwapuuza kutokana na ubora wa uwanja huo kuandaa mechi kubwaa kama hiyo ila wakapuuza kabisaa.

Kulingana na katibu mkuu wa kilabu ya Gor mahia Nicanor Arun ni kwamba hawatachezea tena uwanjani humo siku zijazo wakilaumu mashabiki wa Shabana kwamba ndio walianza vurugu hiyo ugani Gusii.

Katibu huyo aliendelea kusema alishangaa licha ya kamanda wa mechi hiyo kutaka mechi hiyo kuhairisha viongozi wa Shabana walisisitiza mechi iendelee kama ilivyopangwa.

Takwimu ambazo zimetolewa na maafisa wa usalama ni kwamba zaidi ya watu 72 waliweza kutibiwa baada ya kujeruhiwa kwenye vurumahi hio kogalo wakiponyoka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao Shabana.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending