Connect with us

News

Gataya: Kaunti ya Kilifi Imeonyesha Kuwajibika Kisheria

Published

on

Kamati ya utekelezaji wa sheria katika bunge la Seneti imefanya kikao na Gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Mung’aro kutathmini jinsi serikali ya kaunti hiyo inavyoendana na sheria za kitaifa.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mwenda Gataya amesema kati ya kaunti ambazo kamati hiyo imezitembelea, serikali ya kaunti ya Kilifi imeonyesha kuwajibika katika kuzingatia sheria.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kikao hicho katika makao makuu ya Gavana wa Kilifi, Gataya ambaye pia ni Seneta wa kaunti ya Tharaka Nithi, amesema hatua hiyo imesaidia kuzuia mivutano ya kisheria.

“Tumefurahishwa na kaunti ya Kilifi jinsi ilivyofuata sheria na katiba na kama kamati ya seneti tumeridhia hatua hiyo kwamba kaunti ya Kilifi ni kati ya kaunti bora zaidi kwa kufata sheria na ndio matarajio yetu. Tumeangalia matumizi ya hazina ya wadi pamoja na zengine na kweli ni wazi kwamba imezingatia sheria kwa kuhusisha umma”, Gataya.

Kwa upande wake Gavana wa Kilifi Gedion Mung’aro amesema wanalenga kubuni sheria itakayowawezesha wasimamizi wa vijiji kutambulika kisheria, sawa na kubuni sheria itakayojumuisha wananchi katika ujenzi wa shule za Chekechea ili kudhibiti matumizi mabaya ya fedha pamoja na kubuni sheria itakayosimamia bodi ya ukusanyaji ushuru wa kaunti.

Wakati huo huo Gavana Mung’aro amedokeza kwamba tangu achukue hatamu ya uongozi, kaunti ya Kilifi imefaulu kurejesha zaidi ya shilingi bilioni 1.9 kutoka kwa kesi mbalimbali zilizowasilishwa Mahakamani, akisema ni lazima sheria izingatiwe.

“Kuna kesi moja hii kaunti ilikuwa inadaiwa milioni 926 na nikapambana hadi milioni 114, moja ilikuwa bilioni 1.1 na kuenda Mahakamani na tukashinda hiyo kesi na labda wakate rufaa na tupate taarifa kutoka Mahakamani lakini kesi hiyo tulishinda kwa hivyo kaunti imepata bilioni 1.1 pamoja na milioni 800 hiyo ni bilioni 1.9”, Mung’aro.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending