Sports
Florian Wirtz Sasa Ni Mali Ya Liverpool

Ni Rasmi kwamba kilabu ya Liverpool imetangaza kupata sahihi ya kiungo wa taifa la Ujerumani na kilabu ya Bayern Leverkusen Florian Wirtz kwa dau la Euro milioni 150.
Mchezaji huyo anakua sajili wa pili kwa kocha Arne Slot na mchezaji ghali katika historia ya kilabu hiyo na miongoni mwa wachezaji 10 waliosajiliwa na donge nono zaidi barani ulaya nyuma ya Neymar na Mbappe ambao wote sajili zao zilikua za kihistoria.
Tineja huyo mwenye umri wa miaka 22 alishinda mataji matatu msimu wa mwaka 2023/24 chini ya kocha Xabi Alonso akifanikiwa kucheka na wavu mara 57 kutoka mechi 197 na kupiga pasi 65 kwa wenzake.
Wirtz anakua ndiye mchezaji ghali wa taifa la ujerumani na ligi ya Bundesliga akiwa pia ghali kusajiliwa ligi ya Epl.
Sports
Florian Wirtz Sasa Mambo Nywee! Kutua Liverpool

Kilabu ya Liverpool imeafikia makubaliano na Bayern Leverkusen kuhusiana na usajili wa kiungo mbunifu Florian Wirtz uhamisho ambao ni rekodi mpya wa uhamisho Uingereza.
Timu hizo mbili zimekua kwenye mazungumzo na sasa kitita cha pauni milioni 116 imeafikiwa kwa tineja huyo mwenye umri wa miaka 22.
Raia huyo Ujerumani sasa atawasili Liverpool kwa ajili ya vipimo vya kimatibabu wiki ijayo na baadaye kutiwa wino kandarasi mpya
Inaaminika Wirtz atamwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds na kuwa sajili wa pili kwa kocha Arne Slot baada ya kupata sahihi ya beki Jeremie Frimpong wa taifa la Uholanzi kwa pauni milioni 29.5.
Sports
Thomas Frank Kocha Mpya Spurs

Kilabu ya Tottenham HotSpurs ya Uingereza imemtambulisha Thomas Frank kuwa kocha mpya kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu mwezi jana licha kushinda kombe la Europa ligi na kilabu hiyo wakishinda Manchester United goli 1-0.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 51 amemwaga wino kwenye karatasi mktaba wa miaka mitatu na kilabu hiyo ya London Kaskazini huku kibarua cha kwanza ni kutoa kilabu hiyo kutoka nafasi ya 17 Epl na kurejesha katika ubora wake.
Raia huyo wa Denmark amekua na kilabu ya Brenford kwa miaka saba na aliwasaidia The bees kumaliza ya kumi msimu jana na alama 56 ligi ya Epl na amekua akiwindwa ni vilabu kadha wa kadha.