Connect with us

Entertainment

Diamond Amshtaki Ex Wake Kwa Kutumia Picha Za Zamani Kum’blackmail

Published

on

Mmiliki na mjasiriamali wa lebo ya Wasafi Media na WCB Wasafi, Diamond Platnumz ameelekea mahakamani kumshtaki mpenzi wake wa zamani kwa kile alisema kwamba anatumia picha za zamani wakiwa pamoja kumchafulia jina.

Akithibitisha hatua hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond alisema kwamba mwanamke huyo ambaye hakuweka wazi utambulisho wake amekuwa akimchafulia jina kwa kutumia video za zamani wakiwa pamoja.

Msanii huyo alithibitisha kwamba ameona baadhi ya video hizo zikisambazwa na mpenzi wake wa zamani mitandaoni kwa lengo la kumharibia jina licha ya kuachana muda mrefu uliopita.

“Nimeona kuna clip zinasambazwa mtandaoni zinazonihusu…clip hizo ni za zamani, mwaka 2023, na zina zaidi ya miaka miwili nyuma…na mwanamke huyo pia niliachana nae takriban miaka miwili sasa,” Diamond alisema.

Msanii huyo alieleza kwamba video hizo zinalenga kumharibia hata penzi lake la sasa na Zuchu, akiweka wazi kwamba alishamjulisha mpenzi wa sasa kuhusu kumalizika kwa penzi hilo la zamani.

“Lakini pia nilimueleza mwenzangu niliye nae na tukasameheana na kuanza maisha mapya…” alisema.

Baada ya kugundua kwamba lengo la mwanamke huyo kutumia video hizo za zamani wakiwa pamoja ni kumharibia, Diamond alisema tayari amelikabidhi mikononi mwa idara husika kisheria.

“Mwanamke huyo sasa ameamua kutumia clip hizo na kuambatanisha na jumbe za uongo kwa lengo la kuni blackmail na kutengeneza fedha, jambo hili lishafikishwa katika mamlaka husika na taratibu za kisheria zinafuatwa. Shukran,” alisema.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Paula Kajala Afunguka Sababu ya Kumtema Rayvanny

Published

on

Mwanamitindo na mtangazaji maarufu kutoka Tanzania, Paula Kajala, hatimaye amevunja ukimya na kueleza sababu za kuachana na msanii nyota Rayvanny.

Katika mahojiano ya wazi, Paula alifichua kuwa uhusiano huo haukuweza kudumu kwa sababu ya kile alichokitaja kama kukosa uthabiti na kutoheshimu hisia za wanawake kwa upande wa msanii huyo.

Paula alisema kuwa safari yake ya mapenzi na Rayvanny ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

“Hajali hisia za mtu yeyote. Alikuwa na Fahima, akaja kwangu, baadaye akaonekana na Feza, na sasa amerudi tena kwa Fahima. Hivyo basi, msishangae kesho mkimuona na mwanamke mwingine. Kwake yeye ni kiki na kubaki trending tu,” Paula alieleza.

Kulingana naye, mabadiliko ya mara kwa mara ya msanii huyo kati ya wanawake mbalimbali yalifanya iwe vigumu kujenga mustakabali thabiti wa pamoja.

Paula alitumia nafasi hiyo kuonya wanawake wanaotamani kuwa na uhusiano na watu mashuhuri kama Rayvanny kuchukua tahadhari.

“Wanawake wanapaswa kuchunguza tabia ya mwanaume kabla ya kuingia kwenye uhusiano. Kwa Rayvanny, mara nyingi huwa ana wanawake kadhaa kwa wakati mmoja,” aliongeza.

Kauli za Paula zilisambaa kwa kasi mitandaoni, zikizua mjadala mpana kuhusu changamoto za kuwa na uhusiano na wasanii wakubwa.

Wengi walihoji kama maisha ya umaarufu yanaweza kuendana na mahusiano ya kudumu, huku wengine wakiona kuwa tabia ya Rayvanny ni taswira ya changamoto zinazowakabili wanawake wengi wanaojaribu kujenga familia na wanaume maarufu.

What do youy think?

Continue Reading

Entertainment

Good Morning to All Dianas, Aandika Diana Yegon Baada ya Kauli ya Pastor Ezekiel

Published

on

Mwanahabari na mke wa Presenter Kai, Diana Yegon, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kuandika ujumbe wa ucheshi uliolenga wanawake wote wanaoitwa Diana.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diana aliandika:

“Good morning to all ladies called Diana. Naskia sifa zetu nzuri nzuri sana. 😁”

Kauli hii imetafsiriwa na mashabiki wake kama jibu la kifahari na la utani kwa maneno ya Pastor Ezekiel, ambaye siku za hivi karibuni alizua mjadala mkubwa baada ya kudai kwamba wanawake wenye jina Diana ni wenye tabia zinazoweza kuvuruga ndoa.

Katika mahubiri yake, Pastor Ezekiel alisikika akisema:

“Ukioa mwanamke anaitwa Diana uishi na yeye, jua yeye ndiye ataku-control kama robot, ndiyo hiyo ndoa idumu… Yeye ndiye atakuwa husband, lakini wewe ukiwa mume, Diana hawezi dumu kwa ndoa… Pia jua ukioa Diana, lazima utashare na watu, sababu jina Diana imebeba mapepo… Hiyo ni ukweli mtupu!!!”

Kauli hii ilisambaa kwa kasi mitandaoni, huku ikiwasha mjadala mpana kuhusu imani, mitazamo ya kijamii na namna majina yanavyohusishwa na tabia za watu.

Badala ya kuingia kwenye malumbano, Diana aliamua kutumia uchemfu na ucheshi kujiweka mbali na mitazamo hiyo. Ujumbe wake wa “Good morning…” ulionekana kama njia ya: Kujipa nguvu na kuonyesha kujiamini kama mwanamke, Kuwatia moyo wanawake wote wanaoitwa Diana ambao huenda walihisi kushutumiwa na kauli ya mhubiri huyo, Kupunguza ukali wa mjadala kwa kutumia mzaha na mtindo wake wa kawaida wa kuchekesha mashabiki.

Mara baada ya posti hiyo, sehemu ya maoni ilijaa vicheko, pongezi na mijadala mikali. Wengi walimpongeza Diana kwa kuchukua hatua ya kugeuza maneno ya ukosoaji kuwa kicheko, wakisema kuwa huo ndio mfano wa kujua thamani yako bila kuyumbishwa na mitazamo ya nje.

Wengine walihoji uhalali wa kauli za kiroho zinazohusisha majina na tabia, wakisisitiza kuwa utu wa mtu hautokani na jina lake bali na malezi, maamuzi na imani.

Mjadala huu unaakisi hali halisi ya jamii ya sasa, ambapo mitazamo ya kidini, mila na maoni binafsi mara nyingi huibua tafsiri tofauti.
Kwa upande mmoja, kuna wale wanaoamini kabisa nguvu za majina, na kwa upande mwingine, kuna kizazi kipya kinachoona jina si kigezo cha utu wa mtu.

Kwa Diana Marua, kauli yake imezidi kuimarisha taswira yake kama msanii na mwanamke jasiri ambaye hajivunji moyo na maneno ya kukatisha tamaa.

Continue Reading

Trending